Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas), Prof. Ephata Kaaya. Kwa mara ya kwanza nchini na katika ukanda wa Afrika
Mashariki na Kusini, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi
Muhimbili (Muhas), kimetoa wahitimu wa shahada ya uzamili katika fani
ya afya ya mazingira na kazi.
Alisema shahada hiyo inawaandaa wahitimu kuwa na ujuzi na maarifa
ya kutosha kukabiliana na changamoto nyingi katika kuhifadhi afya za
viumbe hai, hususan katika mazingira ya kuishi na kufanyia kazi
yanayoweza kusababishwa na kemikali, hewa, maji, vyakula na udongo.
“Wahitimu hawa watakuwa na uwezo wa kutambua, kutathmini, kudhibiti
hatari za afya katika mazingira ya kuishi na kufanyia kazi,” alisema.
Alisema maeneo ambayo yatanufaika kwa kuwatumia wataalam hao ni pamoja
na vyuo vya elimu ya juu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, serikali za
mitaa, mamlaka ya afya na usalama kazini, Mfuko wa Fidia kwa
Wafanyakazi, shughuli za migodi mikubwa, na viwanda vikubwa.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la chuo hicho, Deogratius
Ntukamazina, aliiomba serikali iendelee kukifadhili chuo hicho na
kupanua miundombinu yake hususani kumalizia ujenzi wa Kampasi Kuu ya
Mlongazila ili kufanikisha majukumu ya chuo kwa ufanisi.
“Kampasi hii itakapomalizika chuo kitaweza kuongeza idadi ya
wanafunzi kutoka 3,500 waliopo sasa hadi zaidi ya 15,000 na hivyo
kuongeza rasilimali watu kwenye sekta ya afya katika ngazi zote,”
aliongeza kusema.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment