Social Icons

Pages

Thursday, December 18, 2014

TPDC: MISHAHARA HAIJAOMBWA KWA WATUMISHI WOTE



Siku moja baada kuibuliwa pendekezo na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuongeza mishahara watumishi wake, Mkurugenzi wa Masoko wa TPDC, Joyce Kisamo amesema fedha hizo hazijaombwa kwa ajili ya wafanyakazi wote na ametetea viwango hivyo kuwa vipo chini ya hali halisi ndani ya sekta ya gesi na mafuta nchini.

Akifafanua pendekezo hilo katika warsha ya siku mbili iliyoandaliwa na shirika hilo jana na kuhusisha watumishi wa Serikali na vyombo vya habari, Kisamo alisema mishahara hiyo imeombwa kwa ajili ya watumishi maalumu watakaosimamia mradi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.
Alisema watumishi hao watakuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu ya kushinda porini kwa zaidi ya siku 28 na kwamba uamuzi wa TPDC kuomba kiwango hicho cha fedha uliangalia ushindani wa malipo katika soko. Alisema kuna wakati walitangaza kazi kwa mameneja wa mradi huo, wengi walijiunga na TPDC kutoka Songas, lakini baadaye baadhi walirudi walikotoka kutokana na walichotakiwa kulipwa kuwa chini ya matarajio. “Watu wanashindwa kuelewa, fedha hizi hatujaomba kwa ajili ya wafanyakazi wote ila ni kwa wale watakaohusika kuendesha na kurekebisha mitambo ya usafirishaji gesi ambayo tumeigharimia kwa fedha nyingi. “Mtumishi huyu anafungiwa kwenye mitambo ili umeme usikatike au usumbufu wowote usitokee, hivi Sh12 milioni kwa mwezi na familia yake inamsubiria inatosha…mimi bado kwangu ni kidogo,” alisema Kisamo.familia yake inamsubiria inatosha…mimi bado kwangu ni kidogo,” alisema Kisamo.
Jana gazeti dada la The Citizen lilibainisha kuwa TPDC kupitia mpango wa mradi wa kusafirsha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam imeomba kuwaongezea mishahara watumishi wake ambapo mtumishi wa kima cha chini atatakiwa kulipwa Sh5.4 milioni na Ofisa Mkuu Mtendaji kulipwa Sh36 milioni kwa mwezi. Pia, Watumishi hao katika pendekezo hilo lililopelekwa Septemba kwa Baraza la Kutetea Walaji la Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura-CCC), watapatiwa marupurupu manono mbali na mishahara hiyo. Watumishi wa kati wa shirika hilo, nyaraka hiyo inapendekeza walipwe kati ya Sh12.6 milioni hadi Sh28 milioni kiasi cha kuwafanya wafanane na maofisa Watendaji wa juu wa kampuni wanaolipwa vizuri nchini.
Hata hivyo, Baraza la Kutetea Walaji la Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura-CC) limeliita pendekezo hilo la mishahara kuwa ni la “kusadikika” na “lisilo na uhalisia”. Huku akionyesha kusikitishwa na kupingwa pendekezo hilo, Kisamo alisema kiwango hicho kitakachotolewa kwa watumishi hao maalumu ni kidogo sana na wala hakifafanishwi na kile wanacholipwa baadhi ya watalaamu wengine katika kampuni nyingine zilizopo ndani sekta hiyo nchini.
Aliongeza; “sisi tumeangalia industry (tasnia) ya ndani pekee na hiki kiwango tulichoomba kimeshushwa na hakifanani hata kidogo na inayolipwa na Songas. Nimeongea na Ewura na kuwaleza kuwa ‘tungediscuss’ (tungejadili) kabla ya kupelekwa nje kwenye mitandao.” Alisema kutokana na mashaka hayo wananchi wanaweza wakalikataa ombi hilo na kusababisha kuwakosa watalaamu ambao wangesimamia mitambo hiyo ya usafirishaji ambayo bila kusimamia na kuhudumiwa mara kwa mara itaharibika mapema.

CHANZO: MWANANCHI

No comments: