Jeshi la Polisi Kanda Maalumu jijini Dar es Salaam
limezuia maandamano ya vijana waliopitia mafunzo ya Jeshi la Kujenga
Taifa (JKT) na kuwataka Kuteua viongozi watano kwenda Ikulu kwa Rais
Jakaya Kikwete kuwakilisha malalamiko yao.
Vijana hao ni waliopitia operesheni Mkapa, Utandawazi, Jiajili, Miaka
40, Kasi mpya, Maisha bora, Uadilifu pamoja na Kilimo kwanza toka mwaka
2000 hadi 2014.
Vijana hao zaidi ya 300 walianza maandamano hayo saa mbili asubuhi kutoka Jangwani kuelekea Ikulu wakiwa wamebeba bendera zenye rangi nyekundu na vyeti walivyohitima mafunzo yao na walipofika eneo la Hospitali ya Ocean Road, polisi walizuia maandamano hayo na kuwataka kuchagua viongozi watakao wawakilisha.
Vijana hao zaidi ya 300 walianza maandamano hayo saa mbili asubuhi kutoka Jangwani kuelekea Ikulu wakiwa wamebeba bendera zenye rangi nyekundu na vyeti walivyohitima mafunzo yao na walipofika eneo la Hospitali ya Ocean Road, polisi walizuia maandamano hayo na kuwataka kuchagua viongozi watakao wawakilisha.
Askari hao waliwataka wengine kuondoka eneo hilo na kutafuta eneo
lenye usalama kwenda kuwasubiri viongozi wao watakapotoka Ikulu na
kuwaletea majibu.
Mmoja wa kiongozi wa mafunzo, Magesa Maijo, alisema lengo la maandamano
yao ni kupeleka kilio chao kwa Rais kutokana na kutopewa majibu
sahihi kwa wizara husika.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment