Ifahamike kuwa kila kampuni ya uchapishaji wa
magazeti au vitabu na kampuni za televisheni na redio huwa na mtindo wao
wa kuandika au kutangaza habari ambao ni tofauti kidogo na vyombo
vingine katika matumizi ya lugha ya Kiswahili.
Hata hivyo ziko mbinu ambazo ni za jumla kwa kila mwandishi ambazo hana budi kuzifuata kama kwa mfano matumizi ya tahajia ya maneno, miundo ya sentensi na mpangilio wa maneno. Tofauti zinazojitokeza ambazo hutumiwa na wachapishaji ama wa magazeti au wa vitabu zinazojulikana kama ‘House style’ ni ndogo na haziwezi kuathiri sana uandishi kwa jumla.
Hata hivyo ziko mbinu ambazo ni za jumla kwa kila mwandishi ambazo hana budi kuzifuata kama kwa mfano matumizi ya tahajia ya maneno, miundo ya sentensi na mpangilio wa maneno. Tofauti zinazojitokeza ambazo hutumiwa na wachapishaji ama wa magazeti au wa vitabu zinazojulikana kama ‘House style’ ni ndogo na haziwezi kuathiri sana uandishi kwa jumla.
Mbinu Bora za Uandishi
Utangulizi
Kwa kuwa waandishi wengi wamesoma katika vyuo
mbalimbali vya uandishi wa habari, imeonekana kuwa kuna haja ya kuwa na
mwongozo wa uandishi bora na aina za mitindo inayotumika na kukubalika.
Mwongozo huu umejikita katika matumizi fasaha na sanifu ya lugha ya Kiswahili ambayo ndiyo msingi katika uandishi wa habari.
Ifahamike kuwa kila kampuni ya uchapishaji wa
magazeti au vitabu na kampuni za televisheni na redio huwa na mtindo wao
wa kuandika au kutangaza habari ambao ni tofauti kidogo na vyombo
vingine katika matumizi ya lugha ya Kiswahili. Hata hivyo ziko mbinu
ambazo ni za jumla kwa kila mwandishi ambazo hana budi kuzifuata kama
kwa mfano matumizi ya tahajia ya maneno, miundo ya sentensi na mpangilio
wa maneno. Tofauti zinazojitokeza ambazo hutumiwa na wachapishaji ama
wa magazeti au wa vitabu zinazojulikana kama ‘House style’ ni ndogo na
haziwezi kuathiri sana uandishi kwa jumla.
Maelezo yafuatayo yametokana na utafiti pamoja na ushauriano baina ya wataalamu wa lugha.
Maelezo
Msingi wa maelezo yaliyoandikwa umezingatia
miongozo iliyowahi kutolewa na Baraza la Kiswahili la Taifa (Bakita)
siku za nyuma kama ilivyoandikwa katika machapisho yao kama kitabu cha
“Jifunze Kiswahili Uwafunze Wengine,’ pamoja na ‘Mwongozo wa Uandishi’.
Kwa kuanzia ningependa kufafanua baadhi ya maneno
yanayokanganya kiasi fulani wasomaji wengi kutokana na kushindwa
kuyapambanua. Sababu kubwa ya mkanganyiko huu ni athari ya lugha za
asili katika Kiswahili sanifu pia ni misingi mibovu wa sarufi ya
Kiswahili inayosababishwa na walimu wa shule za msingi wasiokuwa na
ujuzi wa kutosha katika taaluma katika fani ya Fonolojia, Fonetiki,
Mofolojia, Semantiki na Sintaksia. Pia wako wale wanaoathiriwa na lugha
za kigeni kama Kiarabu na Kiingereza. Lugha hizi za kigeni kimetufanya
tuione lugha ya Kiswahili kama chotara wa lugha nyingine wakati lugha
hii ina misingi ya lugha ya Kibantu. Nitaanza kufafanua baadhi ya maneno
nna vifungu vya maneno kwa utaratibu wa kutumia alfabeti. Kwa mfano:
A
Ajali/ajari: Ajali ni tukio lenye madhara yanayotokea ghafla. Ajari ni malipo kwa kazi ya ziada na jina
linalofahamika ni ovataimu ambalo limetoholewa kutoka katika neno la
Kiingereza la ‘overtime’.
Aidha/au /ama:
Aidha/au /ama:
Neno aidha asili yake ni Kiarabu na tangu likopwe, matumizi yake hayajabadilika. Kuna wakati tunalitumia kama waaidha. Watumiaji
wengi wanafuata mtindo wa Kiingereza wa ‘either ... or’. Tunasoma kwa
mfano: “Wataalamu wa Kichina watabaki aidha bara au visiwani. Matumizi
sahihi ni “Wataalamu wa Kichina watabaki ama bara au visiwani.
Maana ya aidha ni tena, basi, zaidi ya hayo, vilevile. Kwa mfano:
Kabla ya kwenda sokoni nitapitia aidha benki kuchukua fedha.
Ahirisha/hairisha: Neno sahihi ni ahirisha. Kuahirisha maana yake ni kuchelewesha jambo kwa makusudi ili lifanyike baadaye.
Adhima/azma: Neno adhima si neno sahihi la Kiswahili ila liko
neno adhimisha ambalo maana yake ni kufanya sherehe ya kukumbuka kwa
tukio fulani kama vile siku ya kuzaliwa, siku ya kufunga ndoa, siku ya
kupata uhuru, n.k.
Neno lingine linalofafana na hilo ni adhimu ( kiv) –enye sifa, iliyotukuka, tukufu, jalili.
B
D
Azma ni jambo linalokusudiwa kufanywa, makusudio au lengo. Wakati mwingine huandikwa kama azima.
Alimradi/ilimradi: Haya ni maneno yenye maana moja. Maana yake ni ili, iwapo, kwa masharti kwamba, mradi.
Aidha: Maana ya aidha ni vilevile, pamoja na hayo, pia,
isitoshe n.k. Kuna wakati tunachanganya aidha na au katika sentensi
moja. Hii inatokana na athari ya Kiingereza ya kutumia ‘either … or’...
Kwa usahihi inatakiwa iwe ‘ama / au’ tunapotaka kulinganisha mambo.
B
Budi: Neno hili likisimama peke yake lina maana ya
hiari. Tukisema ,”Wakulima ni budi walime” tuna maana kuwa wakulima ni
hiari walime.Tunatakiwa kusema “Wakulima ni lazima walime au wakulima
hawana budi kulima. Kwa usahihi tunasema “Wakulima hawana budi kulima”
(yako maneno yanayofanana kimuundo kama sina budi, hatuna budi, hawana
budi , huna budi)
Baadaye/baadae: Neno sahihi ni baadaye
D
Digiti/Digitali: Digiti ni nomino na limetoholewa kutoka kwa neno ‘digit’ lenye
maana ya tarakimu. Neno hili ni nomino na ni sahihi. Digitali ni kisifa
(adjective). Kwa kawaida tunatohoa nomino na wala siyo kisifa. Hivyo
neno sahihi ni ‘digiti”.
F
G
H
I
J
Durusu/rudufu: Haya ni maneno yanayochanganywa na yana maana tofauti. Kudurusu ni kupitia tena maandishi yaliyoandikwa kwa madhumuni ya kusahihishwa au kuboreshwa na kutoa toleo jipya.
Rudufu ni kufanya nakala, kufanya kitu madhubuti k.v kurudufu nyuzi kuwa imara.
Darubuni: Ni chombo cha kuonea mbali; kionea mbali yaani ‘Telescope/binoculars’.
Dahili/sajili: Maana ya kudahili
ni kutaka kujua habari za watu kwa kuulizauliza au kudadisi. Kusajili ni
kuweka orodha ya kmbukumbu za vitu au watu kwa kuviandika katika
daftari maalumu.
F
Fedha/pesa/hela: Haya ni maneno yenye maana moja lakini yana asili
tofauti. Maneno mengine yanayofanana na hayo ni sarafu, fulusi, faranga
ambayo hutumika katika malipo. Maneno yote yanakubalika. Hata hivyo tuna
mazoea ya kutumia neno fedha upande wa bara na pesa upande wa visiwani.
Fikiri /dhani: Maneno haya yanafanana kwa kiwango fulani lakini
wengi wetu huyachanganya na kuyatumia kama visawe. Yana tofautiana
kidogo. Fikiri ni kutumia ubongo kutatua jambo, kutafakari, kuwaza.
Kudhani ni kufikiri bila kuwa na uhakika.
G
Ghairi: Kuacha kutenda kilichokusudiwa.
Ghushi/gushi: Neno sahihi ni ghushi
H
Hadubini: Ni chombo cha kuona vitu visivyoonekana kwa macho (Microscope).
Hoteli/mahoteli: Neno sahihi ni hoteli.
Hovyo/ovyo: Neno sahihi ni ovyo. Digiti ni nomino na limetoholewa kutoka kwa neno ‘digit’ lenye
maana ya tarakimu. Neno hili ni nomino na ni sahihi. Digitali ni kisifa
(adjective). Kwa kawaida tunatohoa nomino na wala siyo kisifa. Hivyo
neno sahihi ni ‘digiti”.
Hadhari/Tahadhari: Hadhari ni nomino na tahadhari ni kitenzi. Hadhari
ni uangalifu. Hadhari kabla ya athari/hatari. Tahadhari ni kitenzi.
Kuepuka jambo ili usipatikane na hatari au ubaya.
Hatima/ hatma: Neno sahihi ni hatima
Harusi/arusi: Maneno yote mawili yanatumika ila kwa mazoea ya wengi neno harusi ndilo linalotumika zaidi.
I
Idadi/nambari: Idadi ni jumla ya vitu au mambo yanayohesabika.
Nambari limetokana na neno namba (number) yana maana ya tarakimu kama 1,
2, 3, 4, 5. Idadi ni namba au hesabu ya kujumuisha.Tunasema idadi kubwa ya Watanaznia ni wakulima.
J
Jingine/Lingine: Yote ni sahihi ila hutegemea muktadha husika.
Jinsi na jinsia: Jinsi ni namna kitu kilivyo au kiumbe kama vile
binadamu, wanyama au ndege. Tunayo jinsi ya kike na jinsi ya kiume. Kwa
lugha ya kigeni ni ‘sex’.ku. Jinsia ni hali ya kuwa mume au mke. Masuala yanayohusiana na mwanamume na mwanamke. Kwa lugha ya kigeni ni ‘gender’.
K
Kuwapo /Kuwepo: Neno linalosadifu ni kuwapo ijapokuwa kwa mazoea watu wengi wanatumia kuwepo.
Kiwanda/Karakana: Kiwanda ni mahali penye sehemu za kuundia vitu
mbalimbali kama milango, vioo, madirisha, magurudumu, n.k. Sehemu hizi
hufahamika kama karakana. Hivyo kiwanda huwa ni mkusanyiko wa karakana
mbalimbali.
Kampuni/Makampuni: Neno sahihi ni kampuni na wala siyo makampuni.
Kurudufu: Maana yake ni kunakili au kutoa nakala nyingine.
Kimbiza /Wahisha: Kukimbiza ni kufuata kitu au mtu kwa mbio nyuma
au kufukuza. Kuwahisha ni kutenda jambo mapema kabla halijaharibika.
Waandishi wanatumia ‘kukimbiza badala ya
kuwahisha.
Kuongea/kuzunguma: Tofauti kati ya maneno haya ni ndogo sana. Kuongea
ni kushiriki katika mazungumzo. Kuzungumza ni kusema maneno katika
mkutano au kwenye mjadala au baraza na kutoa maoni.
Kupeleka: ni kuchukua kitu au mtu
na kukifikisha/kumfikisha mahala fulani. Tukiongeza kiambishi cha –ea
tunapata kupelekea kwa maana ya kufikisha kitu kwa niaba ya…Mtoto
alimpelekea mzazi wake mbegu shambani. Hivi sasa matumizi ya pelekea
yanaleta kichefuchefu kwa Waswahili.
Kuyeyuka/kuyayuka: Neno sahihi ni yeyuka kwa maana ya kugeuka kwa kitu kigumu kuwa kioevu.
Kunyauka/kukauka: Kunyauka ni kufifia kwa sababu ya ukame au joto. Kukauka ni kutoka maji na kuwa kavu
Kengeuka: Kwenda kombo, angamia. Kengeua ni kumfanya mtu afuate njia mbaya au tabia mbaya, kupotosha.
Kutokana/Kufuatia: Maneno haya
mawili yanatumika kama vile yana maana moja. Kwa kweli yana maana
tofauti kabisa. Kwa mfano tunasema,” Kutokana na njaa kali inayowakabili
wananchi wa Bariadi, serikali imepeleka magunia 20,000 ya mahindi. Ni
makosa kusema, “ Kufuatia njaa kali inayowakabili wananchi wa Bariadi,
serikali imepeleka magunia 20,000 ya mahindi.
Kugharamia/kugharimia:
Neno sahihi ni kugharimia badala ya kugaramia. Gharama ni nomino.
Kwa ujumla/kwa jumla:
Maneno yote yanatumika kutegemeana na
maudhui.Tunasema kwa jumla maisha ni magumu. Hata hivyo neno linatumika
kama: Kwa ujumla wake mvua imekithiri. Ni makosa kutumia, ‘Kwa ujumla
tumefanikiwa…bali kwa jumla tumefanikiwa.’
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment