Wanafunzi wakishiriki usafi wa mazingira shuleni. Baadhi ya wazazi
wanasema shule za bweni si mwafaka kwa wanafunzi wadogo kiumri.
Hivi karibuni, serikali ya Rwanda imepiga
marufuku shule za bweni kwa wanafunzi wa elimu ya msingi. Wizara ya
Elimu ya nchi hiyo, imetoa muda wa miaka mitatu kwa shule za msingi za
bweni kufunga huduma hiyo. Lengo la Serikali ya Rwanda ni kutaka kuona watoto
wakipata muda zaidi wa kukaa na wazazi wao, kuwafinyanga kimalezi mpaka
wafikie umri wa kujitambua zaidi.
Hivyo kwa serikali ya Rwanda muda mwafaka wa wanafunzi kwenda shule za bweni ni pale wanapofika sekondari.
Upepo wa shule za bweni kwa wanafunzi wenye umri
mdogo umeikumba pia Tanzania. Hivi sasa kuna idadi kubwa ya shule
zinazopokea wanafunzi chini ya miaka 10 wanaosoma elimu ya msingi. Je,
ni mwafaka kwa Serikali ya Tanzania kufuata nyayo za Rwanda kuzuia shule
hizo?
Utengano na wazazi
Hapa nchini, wanafunzi wanatumia miezi si chini ya
tisa wakiwa shuleni, muda ambao Meneja wa utafiti na uchambuzi wa
sera wa shirika la HakiElimu, Godfrey Boniventure anasema hauwapi watoto
nafasi ya malezi kutoka kwa wazazi
“Miezi tisa ni mingi kwa mtoto kuwa mbali na
malezi ya wazazi, kwa hivyo nakubaliana na mabadiliko ya Rwanda;
ingetokea hapa nchini ingesaidia japokuwa ninaamini haiwezekani
kutokana na changamoto ya umbali wa shule nyingi zilivyojengwa ambazo
zinalazimisha kuwa na bweni japo si vizuri kimalezi,’’ anasema na
kuongeza:
“Kiuzoefu, watoto wengi wanaosoma shule za bweni
huathirika kimalezi; wanabadilika tabia bila mzazi kujua lakini kama
mwanafunzi anakwenda shule na kurudi, ni rahisi kwa mzazi kutambua
mabadiliko na mwenendo wake.”
Anasema hata Korea Kusini ni miongoni mwa mataifa
yaliyoendelea, lakini hayatumii mfumo wa shule za bweni ila kwa
wanafunzi maalumu, kama anavyofafanua:
“Korea Kusini wanatumia shule za bweni kulea
vipaji na si kwa masomo ya sekondari au shule ya msingi, vipaji ndiyo
vinalelewa, kukuzwa ili kulinda visipotee.’’
Katibu Mkuu wa Umoja wa wamiliki wa shule na vyuo
binafsi nchini (Tamongsco), Benjamin Nkonya, anasema uamuzi wa kufungia
shule za bweni kwa daraja la elimu ya msingi ni sahihi.
“Kuanzia kidato cha kwanza mpaka vyuoni
inawezekana kukaa bweni na kwa Tanzania tunaweza kufanya hivyo, lakini
lazima kuwapo na huduma nzuri za usafiri wa mabasi ya wanafunzi kwa
wanafunzi wa shule za kwenda na kurudi nyumbani,’’anasema.
Shule za bweni na maadili
Hoja kinzani
Haja ya shule za bweni
Hata hivyo, Nkonya ambaye pia ni mmiliki wa Shule ya Sekondari
ya King Solomon, anasema uzoefu unaionyesha uendeshaji wa shule za bweni
una nafuu kuliko shule za kutwa
Evelyin Mchau amewahi kusoma katika shule ya
bweni, anaunga mkono kufutwa kwa shule za bweni hasa kwa watoto wa elimu
ya awali na msingi.
“Kuanzia chekechea na shule ya msingi wanatakiwa
kusoma shule za kawaida ili kuwa karibu na wazazi, lakini sekondari kwa
mfano, mimi shule ya bweni imenisaidia kimalezi. Nilikabidhiwa kwa
mwalimu wa malezi ambaye alinifuatilia mwenendo wangu,” anasema.
Shule za bweni na maadili
Mzazi wa jijini Dar es Salam, Maria Mashasi
anasema ameamua kusomesha watoto wake wawili katika shule za kutwa
baada ya kugundua kuwa shule za bweni hazina faida kimaadili.
“Mtoto wangu mkubwa anasoma darasa la pili,
mwingine chekechea, wote wanasoma ABC Capital School iliyopo Kinyerezi.
Sikuona umuhimu kwani nimeshuhudia watoto wa rafiki yangu waliosoma
bweni lakini wameathiriwa na utandawazi. Alitumia gharama kubwa
kuwasomesha lakini waliambulia mimba na uvutaji dawa za kulevya,”
anasema na kuongeza:
“Kinachosababisha wazazi kupeleka watoto bweni ni
hali ya kubanwa na majukumu bila kuona umuhimu wa malezi yao kwa watoto,
kazi haiwezi kuwa bora zaidi ya malezi kwa mtoto,Tanzania tunatakiwa
kufuata Rwanda.”
Hoja kinzani
Mwalimu wa shule ya bweni ya Barbro Johansson,
iliyopo Mbezi jijini Dar es Salaam, Doroster Mandes, anasema uamuzi wa
Rwanda ni sahihi lakini inategemea na mazingira ya shule zake. Kwake
tathmini ya Rwanda inaweza kutofautiana na Tanzania.
“Kuna mwanafunzi anaharibika hata akiwa shule za
kawaida, unakuta mzazi anatingwa na hajui mwenendo wake shuleni. Hilo
pia ni tatizo kwa hivyo kufungia bweni siyo suluhisho kwani kuna shule
zinazotumia misingi mizuri ya malezi,” anaeleza mwalimu Doroster.
Haja ya shule za bweni
Kwa baadhi ya watu, shule za bweni kwa watoto zina
manufaa kadhaa kama vile kuwaepusha watoto na adha ya kutembea umbali
mrefu kwenda na kurudi shule.
Kauli ya Serikali ya Tanzania
“Wazazi wengi wanalazimika kuwapeleka bweni hata chekechea,
shule za msingi kutokana na mateso yaliyopo, yaani mwanafunzi
anaathirika kisaikolojia kabla ya kufika shuleni. Anaamshwa asubuhi na
mzazi, anafika kituoni konda hamtaki, akifika amechelewa anakutana na
bakora za mwalimu, kwa mazingira hayo matokeo yake lazima afeli
mtihani,” anasema Nkonya.
Aidha, wapo wazazi wanaoamini kuwa shuleni ni
mahala mwafaka kwa watoto kuzingatia masomo kuliko nyumbani. Hivyo
kuepukana na ushawishi wanapendelea kuwapeleka watoto shule za bweni
wakiwamo wale wenye umri mdogo wa hata chini ya miaka saba.
Kauli ya Serikali ya Tanzania
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne
Kilango Malecela anasema Tanzania haiwezi kufuata mtazamo au uamuzi wa
Rwanda kufuta shule zinazotoa huduma ya malazi kwa wanafunzi.
“Rwanda ina sababu zake na sisi tumeshaangalia
hilo tukakubaliana nalo. Kila nchi ina changamoto zake kwa hivyo nadhani
hata sisi tuko sawa kwa upande wetu.”
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment