Social Icons

Pages

Friday, June 05, 2015

UFISADI KCMC WATINGA BUNGENI

Mbunge wa Viti Maaalum Chadema, Suzan Lyimo.
Wabunge wamefichua ufisadi katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC, mkoani Kilimanjaro, ambayo watendaji wakuu wa hospitali hiyo wameuziana magari mapya ya serikali kwa bei ya kutupa ya Sh. milioni 8 kila moja.
Ubadhirifu huo ni wa kutisha uliibuliwa jana Bungeni wakati mjadala wa hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa mwaka wa fedha wa 2015/2016. Mbunge wa Viti Maaalum Chadema, Suzan Lyimo, alisema viongozi wakuu KCMC wameuziana magari aina ya Prado na Nissani Patro kwa bei ya Sh. milioni 8 kila moja mwaka 2013, ambayo yalipelekwa katika hospitali hiyo kwa shughuli mbalimbali.
Alisema kutokana na ubadhirifu huo Mhasibu wa hospitali hiyo, Paulo Muhunya, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Afya (TUGHE), alimjulisha Rais Jakaya Kikwete, kwa kumtumia ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kuhusu ufisadi huo. Lyimo alisema katika hali ya kushangaza Mhasibu huyo baada ya kutoa taarifa za ubadhirifu huo, Mei 5, mwaka huu, alisimamishwa kazi jambo ambalo linatia mashaka.
"Nchi hii inashangaza inakuweje mtu aliyesaidia kutoa taarifa za kufichua wizi yeye ndiye anaadhibiwa, au ndio utaratibu wa serikali ya CCM kuwalinda wezi," alisema. Naye Mbunge wa Viti Maalum Chadema, Congesta Lwamlaza, alisema Serikali ya CCM ni ya kutumbua tu ndiyo maana fedha nyingi zinatengwa kwa mambo ya starehe tu.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments: