Social Icons

Pages

Friday, June 05, 2015

AFB YAPOKEA DOLA MIL 20 KUPANUA UWEKEZAJI KUSINI JANGWA LA SAHARA

Mkurugenzi wa AFB, Karl Westvig.
Kampuni ya Huduma za Kifedha ya AFB inayojihusisha na kutoa ushauri na huduma za kifedha kwa wajasiriamali, imeingia mkataba wa Dola milioni 20 na kampuni ya Gemcorp inayojihusisha na uwekezaji wenye mtazamo wa masuala ya kimasoko.Akizungumzia mkataba huo, Mkurugenzi wa AFB, Karl Westvig, alisema: “Nimefarijika sana kuingia makataba huu ambao umekuja kwa wakati mwafaka ambao pia ni muhimu sana kwa kampuni. Uwekezaji huu wenye mantiki kutoka kwa Gemcorp utatoa mchango mkubwa sana katika kuleta maendeleo Kusini mwa Jangwa la Sahara.”
Kwa sasa AFB ipo pia katika mataifa ya Ghana, Kenya, Zambia na Tanzania, huku ikiwa na mpango wa kujitanua katika nchi nyingine za Afrika ifikapo mwaka  2020 ikiwa na bidhaa zenye ubunifu na ufumbuzi na zenye kukidhi vigezo vyote sokoni.
Kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya Dunia, zaidi ya watu milioni 400 waliopo Kusini mwa Jangwa la Sahara bado wanafanya shughuli zao nje ya mfumo rasmi wa kifedha.
Akizungumzia juu ya uwekezaji huo, Mkurugenzi wa Gemcorp, Atanas Bostandjiev, alisema: “Huduma za kifedha ni sekta muhimu kwa mustakabali wa kampuni yetu na tumekuwa tukiangalia hasa soko la Afrika, AFB ni fursa kubwa ya kiuwekezaji kwetu. Ikiwa na lengo la kutekeleza maendeleo ya kifedha kupitia ufumbuzi wa kiteknolojia, kampuni hii inalenga kuharakisha ukuaji wa maendeleo kulingana na mahitaji ya Bara la Afrika hasa kwa tabaka la kati.”
Alisema anaamini kwamba wataendelea kufanya kazi kwa pamoja na kuendeleza ushirikiano kwa maendeleo ya  AFB.

CHANZO: NIPASHE

No comments: