 Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji 
Francis Mutungi amevitaka vyama kurekebisha katiba zao kwenye kipengele 
kinachoruhusu kuanzishwa kwa vikosi vya ulinzi na usalama.
Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji 
Francis Mutungi amevitaka vyama kurekebisha katiba zao kwenye kipengele 
kinachoruhusu kuanzishwa kwa vikosi vya ulinzi na usalama.Vyama vyenye vikosi cha ulinzi na usalama ni Chadema chenye Red Brigade, CCM (Green Guard), CUF (Blue Guard) na sasa ACT-Wazalendo (ACT Amani).
Mutungi alisema uanzishwaji wa vikundi hivyo unakwenda kinyume na Katiba ya nchi inayolipa jeshi la polisi mamlaka ya kulinda usalama wa raia na mali zao.
Akizungumza baada ya mkutano wake na vyama hivyo 
jana, Jaji Mutungi alisema katiba za vyama vingi vilivyosajiliwa kabla 
hajaingia ofisini vilikuwa na kifungu kinachoruhusu kuanzishwa kwa 
vikosi vya ulinzi na usalama wa mali za chama au viongozi wao wawapo 
katika mikutano.
“Haturuhusu kifungu hicho kuwapo kwenye katiba za 
vyama vinavyosajiliwa sasa (hakugusia ACT - Wazalendo). Hatuvifundishi 
vyama vya siasa namna ya kuandaa katiba zao lakini tunasimamia kifungu 
hiki kwa vile kinapingana na sheria.”
Jaji Mutungi alisisitiza kuwa vyama vya siasa 
nchini havina uelewa wa sheria ya vyama vya siasa ambayo ndiyo 
inayovisimamia, ndiyo maana vinashindwa kuendesha shughuli zao kwa 
mujibu wa sheria hiyo.
Kauli ya polisi
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Ernest 
Mangu alisema watapambana na vikundi vya ulinzi na usalama ndani ya 
vyama vya siasa wakati wa Uchaguzi Mkuu endapo vitaingilia majukumu ya 
jeshi la polisi.
Alisema uanzishwaji wa vikundi hivyo ni kinyume 
cha sheria inayolipa Jeshi la Polisi dhamana ya kulinda usalama wa raia 
na mali zao.
Alisema vikundi hivi vilianzishwa kama chipukizi 
au halaiki lakini baadaye vilikuwa na kubadili malengo na kuanza 
kuingilia majukumu ya polisi na kuhatarisha amani.
Maoni ya wadau
Hata hivyo, kauli za Msajili na Mangu zilipokewa 
kwa hisia tofauti na viongozi wa vyama hivyo na baadhi vikiweka wazi 
kuwa havipo tayari kuachana na vikundi hivyo.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM – Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema 
vijana wa Green Guard hawaandaliwi kijeshi na kuwa tishio kama vyama 
vingine, bali kuwafanya wawe vijana bora, wakakamavu na kuwajengea 
uzalendo ndani ya nchi yao.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema chama
 chake hakipo tayari kuivunja Red Brigade huku akiilaumu CCM kuwa 
kikundi chake cha Green Guard kimepata mafunzo ya kijeshi kikifundishwa 
na askari tofauti na wao ambao wanafundishwa na raia.
Akihutubia mkutano wa hadhara mjini Nzega jana, 
Mbowe alisema suluhisho la tatizo hilo haliwezi kuwa sheria bali 
kuhakikisha haki inatendeka na inaonekana kutendeka kwa kila chama, 
akitolea mfano jinsi viongozi wa chama hicho walivyopigwa na Green guard
 bila polisi kuchukua hatua.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
 

No comments:
Post a Comment