Juzi Rais Jakaya Kikwete wakati akipokea Ripoti
ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka
unaoishia Juni 2014, alitoa maagizo makali baada ya kubaini ndani ya
ripoti hiyo kuna madudu mengi ya matumizi mabaya ya fedha za umma.
Kwa jinsi ripoti hiyo ilivyotoa taswira mbaya kwa Serikali kuhusiana na matumizi ya fedha za umma, Rais Kikwete aliamua kuviagiza vyombo vya Serikali kubaini maofisa wote wa Serikali wanaohusishwa na matumizi mabaya ya fedha za Serikali, ikiwa ni pamoja na kutoa malipo bila nyaraka zozote, kutumia fedha nje ya Bajeti na kutoa malipo bila idhini ya ofisa masuhuli, ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.
Kwa jinsi ripoti hiyo ilivyotoa taswira mbaya kwa Serikali kuhusiana na matumizi ya fedha za umma, Rais Kikwete aliamua kuviagiza vyombo vya Serikali kubaini maofisa wote wa Serikali wanaohusishwa na matumizi mabaya ya fedha za Serikali, ikiwa ni pamoja na kutoa malipo bila nyaraka zozote, kutumia fedha nje ya Bajeti na kutoa malipo bila idhini ya ofisa masuhuli, ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.
Pia, Rais Kikwete ameagiza kuchukuliwa kwa hatua
kali za kisheria kwa maofisa wote wa serikali ambao wanahusika kulipa
mishahara hewa kwa watumishi ambao wameacha kazi, wamefariki dunia,
wamestaafu na wanaendelea kulipwa mishahara kupitia akaunti zao za
benki.
Rais pia ameiomba Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi
kuisaidia serikali kuboresha mfumo wa zabuni ambako serikali inapoteza
fedha nyingi kwa kupitia mchakato mrefu mno wa kupatikana kwa wazabuni
wa kutoa vifaa na huduma kwa Serikali.
CAG), Profesa Mussa Juma Assad, aligundua malipo
yasiyokuwa na nyaraka, hati za malipo ambazo hazikuwasilishwa kwa
ukaguzi, fedha iliyotumika nje ya bajeti, matumizi yasiyokuwa na manufaa
(nugatory expenditure) na malipo ambayo hayakuidhinishwa na maofisa
masuuli.
Profesa Assad alimweleza Rais Kikwete pia kuwa
Ofisi yake inapendekeza kuwa taasisi zote za serikali zisiendelee
kununua vifaa na huduma kutoka kwa wafanyabiashara wasiotumia mashine za
stakabadhi za kielektroniki (EDF), stakabadhi ya kukiri kupokea fedha.
Mbali na udhaifu katika maeneo hayo, bado ugonjwa
sugu wa watumishi hewa umeendelea ambapo kwenye ripoti ya CAG ya mwaka
ulioishia Juni 2011, kiasi cha Sh1 bilioni kililipwa kama mishahara kwa
watumishi wa halmashauri ambao hawapo; kutokuwasilishwa kwa vitabu vya
stakabadhi za mapato kutoka halmashauri vyenye thamani ya
Sh4,227,984,618.
Ni dhahiri mwaka baada ya mwaka CAG amekuwa akitoa
ripoti nzuri na mara nyingi kumekuwa na maswali ya umma kwa ujumla
wake, kwamba nini faida ya kuwa na ripoti hizi mwaka baada ya mwaka kama
wahusika hawafanywi lolote kutokana na upungufu yanayojitokeza kwenye
ripoti hiyo?
Tunaviomba vyombo husika kumsaidia Rais Kikwete
kwa kuitekeleza kwa vitendo kauli yake ya kuwachukulia hatua za kisheria
wale wote wanaotajwa ndani ya ripoti ya CAG kwamba wanahusika na
matumizi mabaya ya fedha za umma.
Kuna wakati huko nyuma Rais Kikwete aliwahi kusema
kuwa katika maeneo ambayo ripoti ya CAG inaonyesha dhahiri kulikuwa na
wizi wa fedha za umma kwa watumishi, taarifa ipelekwe polisi na wahusika
washtakiwe.
Sisi tunasema kauli ya Rais Kikwete ni ya kuungwa
mkono kwa kuvitaka vyombo husika kuchukua hatua za kisheria bila
kuchelewa na kwa kutenda haki. Ni muhimu kwa vyombo hivyo kufanyia kazi kwa haraka kauli hiyo ya Rais Kikwete.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment