
Inashangaza kwamba kufikia leo hii, CCM bado inawazuia wanachama wake kutangaza kugombea urais. Chini chini, idadi ya wanaotaka kugombea nafasi hii inaongezeka. Wengine wanataka wenyewe, wengine wanasakiziwa.
Ukweli ni kwamba, ingawa nafasi ya urais ni moja tu, wanaoitamani ni wengi kupindukia. Vyama vingine vimebaki kimya, si kwamba vinazuia mtu kujitangaza labda ni mbinu za kutaka kusubiri kwanza kuona chaguo la CCM ili wajipange. Ila bado hatujasikia tamko la kuwazuia wanachama wa upinzani kujitokeza kugombea kama tunavyosikia kutoka CCM.
Ukweli ni kwamba, ingawa nafasi ya urais ni moja tu, wanaoitamani ni wengi kupindukia. Vyama vingine vimebaki kimya, si kwamba vinazuia mtu kujitangaza labda ni mbinu za kutaka kusubiri kwanza kuona chaguo la CCM ili wajipange. Ila bado hatujasikia tamko la kuwazuia wanachama wa upinzani kujitokeza kugombea kama tunavyosikia kutoka CCM.
Unaweza kuiba, wakafumba macho, unaweza kukosa
uzalendo, wakafumba macho, unaweza kushindwa kuwajibika wakafumba macho,
unaweza kutoa roho ya mtu wakafumba macho, lakini ukitangaza kugombea
urais kabla ya muda, unawekwa kifungoni. CCM wanashangaza! Ukali wanaouonyesha kwa watu wanaojitangaza mapema
unatisha. Wangekuwa wakali kwa mambo mengine ya msingi, Taifa letu
lingekuwa mbele zaidi. Mwaka jana, CCM iliwafungia wanachama wake sita waliojitokeza kujitangaza kugombea.
Wakapata adhabu ambayo hadi leo ni kama inaendelea
maana, hakuna uwazi. Katika dunia ya leo ya sayansi ya teknolojia, bado
mambo yanaendeshwa kama uchawi vile.
Tukihesabu siku, zinakwenda. Tungependa kuwafahamu
wagombea, tungependa kuwahoji na kuyachunguza maisha yao, kuchunguza
imani zao za mambo mbalimbali. Ni muhimu kufahamu mtu anayetaka kugombea uongozi
wa juu katika Taifa anaamini nini? Ana itikadi gani? Anafuata sera gani?
Ni mzalendo au ni kibaraka? Yote haya ni muhimu kufahamika mapema.
Ushawishi wa wananchi
Wagombea wa CCM, hawatoki mwezini. Ni watu
wanaoishi kwenye jamii yetu. Tunawafahamu. Hivyo CCM, haiwezi kukwepa
ushawishi wa wananchi. Hakuna ushahidi wa kutosha unaoonyesha kwamba Halmashauri Kuu inawafahamu vizuri wagombea kuwazidi Watanzania wengine.
Kama CCM inamtafuta mtu wa kuliongoza Taifa, haiwezi kukwepa mapenzi ya watu wote wanachama wa CCM na wale wasiokuwa wanachama. Kama mtu ni fisadi; anajulikana kwa kula rushwa,
anajulikana kwa kufuja hovyo pesa za Serikali, anajulikana kwa kiburi
chake na majigambo, anajulikana kwa kutotumikia bali kutumikiwa.
Anajulikana kwa kutolipenda Taifa lake na kulithamini.
Anajulikana kwa kukaribisha miradi hewa na
kushiriki kuiuza nchi, anatibiwa nje ya nchi, kila kitu chake
kinanunuliwa nje ya nchi na watoto wake wanasomea nje ya nchi,
halmashauri kuu haiwezi kuibadilisha hali yake. Mtu akishazidi miaka 55 ni vigumu kumbalidisha. Samaki hukunjwa angali mbichi!
Kama nilivyosema hapo juu, hawa wagombea hawatoki mbinguni. Tunaishi nao. Kama ni mwanamke, tunawafahamu wanawake wote wa CCM ambao wana sifa, mvuto na uwezo wa kuliongoza Taifa.
Kama ni vijana, tunawafahamu na kusema ukweli vijana wengi wamejitokeza na kuonyesha hamu ya kutaka kuliongoza Taifa lao. Ni wazi vijana wengine hawana historia hata ya
kuandika chochote juu ya maisha yao, juu ya Tanzania au mwelekeo wa
Taifa letu, wanajitokeza kufurahisha watu na kuonyesha kwamba kila
Mtanzania anaweza kuwa Rais.
Hawa wanacheza na wala hatuna ulazima wa
kuwasikiliza au kuwatilia maanani. Kuna vijana wachache, ambao wana
uwezo mkubwa na kusema ukweli mtu ambaye ana miaka zaidi ya 40 siyo haki
kumchanganya na vijana au watoto, huyu ni mtu mzima, baba wa familia na
mtu mwenye wajibu mkubwa kwa familia yake na taifa lake. Hata hivyo, kuna baadhi ya wazee, wale ambao
hawataki kustaafu, wanaotamani kufa wamekikalia kiti cha urais
wamejitokeza pia. Ni wazi wazee hawa wanaongozwa na tamaa ya madaraka.
Nchi yetu imeweka miaka ya kustaafu kwenye umri wa
miaka 60, sasa wazee wanaotaka kugombea urais na wako juu ya miaka 60,
wana matatizo ya aina fulani. Tukishindwa kuwashawishi kustaafu kwa
amani, basi tuwatafutie dawa ya ugonjwa wao.
CHANZO: MWANANCHI
CCM inamtaka nani?
Tunabaki kujiuliza, CCM, wao wanamtaka nani, huyo
ambaye havutii hisia za watu? Maana kama anavutia ni lazima ataonekana
kwa kila mtu. Kama anavutia ni lazima atapata kura za maoni. Atatoka wapi kama siyo miongoni mwa wale wale
tunaowajua na kuishi nao? Atatoka wapi kama si wale wanaopitapita huku
na kule wakisambaza bahasha miongoni mwa wajumbe wa mkutano mkuu?
Dunia nzima inajua jinsi Tanzania, tunavyoishi
kishirikina. Mauaji ya watu wenye ualbino yamelipaka Taifa letu matope.
Watu wanaamini tunaishi kishirikina. Na mwenendo wa CCM wa
kuwanyamazisha wanachama wanaotaka kugombea umekaa kishirikina. Kwani
kuna ubaya gani mtu kujitangaza kutaka kugombea urais?
Akitumia njia mbovu, ikifika kura za maoni,
anatupwa nje. Lakini kufanya mambo kwa mfumo wa kishirikina ni kuongeza
shaka katika mwenendo wa Taifa. Si lengo la makala haya kumpigia debe yeyote yule
anayetaka kugombea kupitia CCM. Ingawa kumpigia mtu debe si dhambi,
maana hii ni nchi yetu sote. Mimi kama Mtanzania na mzalendo wa kweli,
nina lengo la kuwakumbusha vigogo wa CCM kwamba sauti ya watu ni sauti
ya Mungu. Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, alisema kwamba Rais wa
Tanzania, atachaguliwa na Mungu. Na Mheshmiwa Magufuli, akarudia kauli
hiyo mara kwa mara. Ni Mungu gani anayeongelewa asiyepitia kwa watu
wake? Kwa upande wa CCM, Mungu amesema kupitia kwa watu kwamba mtu
mwenye sifa zisizotiliwa shaka ndiye atasimama upande wa CCM . Hiyo
ndiyo sauti ya Mungu. Si maoni yangu, bali ni maoni ya watu tunaowauliza
maoni yao juu ya uchaguzi ndani ya Chama cha CCM. CCM inaweza kuamua
kuziba masikio lakini ukweli utabaki palepale.
Hivyo ni muhimu tukamfahamu mgombea wa CCM mapema.
Tumpime na kumhoji na yeye ajieleze na kujipima na wagombea wa vyama
vingine. Hivi ndivyo nchi zilizoendelea zinafanya.
Hivyo ndivyo nchi zote zinazofuata demokrasia
zinafanya. Wagombea wanafahamika kwa watu zaidi ya mwaka mzima. Huu
mfumo wa kuviziana kama wachawi, inaelekea ni Watanzania tu!
Ni lazima kubadilika ili tuweze kuishi kwenye dunia hii ya Utandawazi ambayo tuna imani kwamba, sasa imekuwa ni kijiji kimoja. Hivyo ni wito wetu kwa CCM, kuwaachia wagombea
kujitangaza, tuwajue na kuwatathmini kama tunavyofanya kwa wagombea wa
vyama vingine.
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment