Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Ummy Mwalimu.
Wakati Tanzania ikitajwa kuwa kichochoro cha
kupitishia dawa za kulevya, wabunge wamehoji dawa hizo zinazokamatwa
kama ushahidi zimekuwa zikipelekwa wapi kwa kuwa haionyeshi kama
zimekuwa zikichomwa moto au la hali inayotia shaka udhibiti wa biashara
hiyo.
Mbunge wa Viti Maalum, Rukia Ahmed, akiuliza swali la nyongeza jana
bungeni, alisema kumekuwa na ucheleweshaji wa kesi za dawa za kulevya
licha ya mtuhumiwa kukutwa na dawa hizo tumboni na pia zilizokamatwa
haionyeshi zinapelekwa wapi.
Alisema kesi nyingi za mauaji na dawa za kulevya zinachukua muda
mrefu kumalizika mahakamani na kusababisha watuhumiwa kukaa zaidi ya
miaka saba rumande na kuhoji kwa nini muda wanaokaa rumande usijumuishwe
kama sehemu ya hukumu wanapotiwa hatiani. Mbunge wa Karagwe (CCM), Gosbert Blandess, alihoji lini serikali
itaanzisha mahakama maalum kwa ajili ya kushughulikia kesi za dawa za
kulevya na rushwa kama njia ya kudhibiti tatizo hilo.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Ummy Mwalimu , alisema
mahakama inaendeshwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za nchi,
hivyo suala la hukumu pamoja na kipindi cha mshtakiwa kutumikia kifungo
chake hufanyika kulingana na sheria inavyotamka kuhusu adhabu ya kosa
husika.
Kuhusu zinapopelekwa dawa za kulevya zinazokamatwa, alisema
kiutaratibu vidhibiti havirudishwi na hukumu ikishatolewa vinateketezwa.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment