
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), Freeman Mbowe (Kulia), akizungumza kwenye kikao cha Kamati
Kuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam jana. Wengine kulia kwake ni
Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, Naibu Katibu Mkuu
(Bara), John Mnyika na Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar), Salum Mwalim.
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), jana ilianza kikao chake cha kufanya maamuzi magumu kuhusu
mambo mbalimbali yanayoendelea nchini ikiwamo kuvurugika kwa uchaguzi wa
Serikali za Mitaa. Kikao hicho maalum cha siku moja, kilifanyika chini ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe jijini Dar es Salaam.
Kikao kilianza saa 5:00 asubuhi kwa wajumbe kupewa taarifa kuhusiana na
kasoro na hujuma zilizotokea wakati wa uchaguzi huo uliofanyika Jumapili
iliyopita nchini kote.
Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa wajumbe pia
walielezwa kamatakamata ya wagombea wa Chadema, wanachama na wafuasi wa
chama hicho inayoendelea nchini kwa kuhusishwa na matukio ya vurugu.
Aidha, wajumbe walielezwa kuwa katika baadhi ya maeneo ambako uchaguzi ulivurugika kutokana na sababu kadhaa zilizosababishwa na wasimamizi wa uchaguzi, uchaguzi umeanza kufanyika kwa kushtukiza bila kuwajulisha wananchi hususani wale ambao walionekana ni mashabiki wa vyama vya upinzani. Afisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene, alisema kikao kitakapomalizika taarifa rasmi ya maamuzi itatolewa leo.
Aidha, wajumbe walielezwa kuwa katika baadhi ya maeneo ambako uchaguzi ulivurugika kutokana na sababu kadhaa zilizosababishwa na wasimamizi wa uchaguzi, uchaguzi umeanza kufanyika kwa kushtukiza bila kuwajulisha wananchi hususani wale ambao walionekana ni mashabiki wa vyama vya upinzani. Afisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene, alisema kikao kitakapomalizika taarifa rasmi ya maamuzi itatolewa leo.
CHANZO:
NIPASHE

No comments:
Post a Comment