Amiri
Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi liliandaliwa na
vikosi mbalimbali wakati wa sherehe ya kuagwa rasmi na vyombo vya ulinzi na usalama.
Vyombo vya ulinzi na usalama vimemuaga rasmi Amiri
Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete, ambaye
anaelekea kumaliza muda wake wa utawala wa miaka 10.
Sherehe za kumuaga Rais Kikwete zilifanyika jana katika Uwanja wa
Uhuru, jijini Dar es Salaam, huku zikiambatana na maonyesho mbalimbali
ya kijeshi. Rais Kikwete alipigiwa mizinga ya heshima pamoja na kukagua vikosi mbalimbali vya majeshi ya ulinzi na usalama.
Aidha, sherehe hizo zilipambwa na shamrashamra za ndege za kivita
zilikuwa zikipita angani huku wanajeshi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania
(JWTZ) wakiwamo makomandoo wakionyesha mbinu mbalimbali za kukabiliana
na maadui pamoja na kuwadhibiti.
Pia Jeshi la Magereza lilionyesha namna ya kudhibiti wafungwa mbele ya Rais Kikwete.
Sambamba na hilo pia Rais alishuhudia namna makomandoo wa jeshi walivyo wakakamavu katika kukabiliana na jambo lolote.
Baadhi ya vikundi vya majeshi yaliyokuwa yakifanya maonyesho mbele
ya Rais Kikwete ni pamoja na JWTZ, Jeshi la Magereza na Jeshi la
Polisi.
Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali
akiwamo Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, Rais wa Zanzibar, Dk.
Ali Mohamed Shein na Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi, Davis
Mwamunyange na Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete.
ATUNUKU NISHANI
RAIS amewatunuku nishani mbalimbali maofisa 30 wa majeshi zikiwamo
nishani ya utumishi uliotukukuka , nishani ya utumishi wa muda mrefu na
nishani ya tabia njema.
CHANZO:
NIPASHE

No comments:
Post a Comment