
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul
Makonda ametakiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu kuwasilisha
utetezi dhidi ya madai ya makada wawili wa CCM, John Guninita na Mgana
Msindai kuwa aliwadhalilisha kwa kuwaita vibaraka wanaotumiwa kuharibu
chama hicho kwa nguvu ya pesa.
Katika kesi hiyo ya madai Namba 68/2015,makada hao wawili wanataka walipwe fidia ya Sh100 milioni kila mmoja, Makonda awaombe radhi na mahakama itoe zuio la kudumu kwa kiongozi huyo wa Serikali kuwazungumzia.
Katika kesi hiyo ya madai Namba 68/2015,makada hao wawili wanataka walipwe fidia ya Sh100 milioni kila mmoja, Makonda awaombe radhi na mahakama itoe zuio la kudumu kwa kiongozi huyo wa Serikali kuwazungumzia.
Awali, Guninita, ambaye alikuwa mwenyeviti wa wa
chama hicho mkoani Dar es Salaam, na Msindai ambaye ni mwenyekiti wa CCM
mkoani Singida, walimtaka Makonda kuwaomba radhi kwa kutoa maneno
ambayo walidai yanawadhalilisha, na kwamba asingefanya hivyo
wangemfikisha mahakamani.
Mahakama ilikuwa imemtaka Makonda, ambaye
anawakilishwa na Lusiu Peter, kuwasilisha utetezi wake leo lakini wakili
huyo aliomba muda zaidi ili aandae majibu ya tuhuma hizo.
Kutokana na maombi ya wakili huyo wa Makonda,
Hakimu Mkazi wa Kisutu, Hellen Liwa, anayeisikiliza kesi hiyo ya madai,
alimtaka mkuu huyo wa wilaya ya Kinondoni kuwasilisha utetezi wake
ifikapo Aprili 23 na kuahirisha kesi hiyo hadi Aprili 27 wakati
itakapotajwa. Katika kesi hiyo, Msindai na Guninita wanaiomba
mahakama hiyo kumuamuru Makonda awaombe msamaha na kumlipa kila mmoja
Sh100 milioni.
Msindai na Guninita wanadai kuwa Makonda
aliwadhalilisha wakati akiwa katibu wa uhamasishaji chipukizi wa UVCCM
kwa kuitisha mkutano na waandishi wa habari na kuwaelezea makada hao
kuwa ni vibaraka wanaotumiwa kuiharibu CCM kutokana na nguvu ya pesa.
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment