Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Prof. John Nkoma.
     
Mfuko wa Mawasilino kwa wote (UCSAT), umeingia 
mkataba na makampuni manne ya simu nchini na kampuni ya satelaiti 
ya Avanti ya Uingereza, kwa ajili ya kusambaza mawasiliano kwenye kata 
102 za vijijini, mtandao kwa shule za serikali 250 na kuunganisha vituo 
na mafunzo ya Tehama 25.
Mkurugenzi wa UCSAT, Peter Ulanga, alisema kata hizo ni kati ya 158 zilizotangazwa, lakini kata 112 zilikubalika na kiasi cha ruzuku ni Sh. bilioni 14.2 pamoja na kata kumi za maradi wa mawasiliano mipakani ambazo zitagharimu Sh. bilioni 2.7.
Mkurugenzi wa UCSAT, Peter Ulanga, alisema kata hizo ni kati ya 158 zilizotangazwa, lakini kata 112 zilikubalika na kiasi cha ruzuku ni Sh. bilioni 14.2 pamoja na kata kumi za maradi wa mawasiliano mipakani ambazo zitagharimu Sh. bilioni 2.7.
Ulanga alisema pia mfuko huo kwa kushirikiana na makampuni hayo 
wameunganisha hospitali saba na sasa wameunda kikosi kazi cha kuangalia 
uwezekano wa kuunga hospitali 150 za wilaya katika huduma ya 
‘telemedicine’.
Alisema pia wako katika hatua ya mwisho ya kusaini makubaliano na 
Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kwa ajili ya 
kugawa kompyuta mpakato kwa wanafunzi walimu ili wanaporudi kazini iwe 
rahisi kufundisha wanafunzi.
Akizungumza na viongozi wa makampuni hayo, Waziri wa Mawasiliano, 
Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa, alisema awamu ya kwanza 
ilihusisha kata 52, ya pili 86 na kwamba serikali inatoa zuruku nusu kwa
 maeneo ya vijijini na mipakani asilimia 100 ikiwa ni utekelezaji wa 
sera ya Tehama ya mwaka 2003 inayoeleza mawasiliano ni haki ya kila 
mwananchi.
Alisema serikali inatambua kuwapo kwa maeneo yasiyo na mvuto 
kibiashara na ndiyo maana inatoa ruzuku ya asilimia 30 hadi 80 ili 
kuwezesha mawasiliano kufika. “Watanzania milioni 12.3 sawa na asilimia 57 ya wenye umri wa miaka
 16 na zaidi wana akaunti za fedha za simu na asilimia 14 ndiyo wenye 
akaunti benki…mawasiliano ni kichocheo cha maendeleo ya uchumi na 
kijamii, yameongeza ajira kwa Watanzania 200,000 kupata ajira za moja 
kwa moja, milioni 1.5 zisizo za moja kwa moja kwa makampuni hayo,” 
alibainisha.
Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Ngodo, alisema mawasiliano 
ni benki, hospitali, elimu, biashara kwa kuwa yanarahisisha na kuwezesha
 utoaji wa huduma ya kusaidia kukuza uchumi kwa kasi kubwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Prof. 
John Nkoma, alisema jamii inapaswa kutumia vizuri mawasiliano na mtandao
 kwani kwa siku za hivi karibuni licha ya kuwapo kwa kasi ya mawasiliano
 pia kuna kasi ya matumizi mabaya ya mtandao.
CHANZO:
     NIPASHE
    
 

No comments:
Post a Comment