Social Icons

Pages

Thursday, April 16, 2015

JANUARY: FEDHA ZIFUATILIWE KAMA ZIMELETA MABADILIKO


Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi, na Teknolojia, January Makamba, amesema ipo haja kwa serikali kufuatilia  fedha zilizotolewa kwenye sekta kadhaa kama zimeleta mabadiliko chanja kwa jamii husika.
Aliyasema hayo jana wakati wa kuwasilikiliza wananchi 400 wanaotoka wilaya mbalimbali nchini ambao watashiriki utafiti wa ushiriki wa wananchi katika maamuzi ya matumizi ya mapato yatokanayo na raslimali za gesi na mafuta ulioandaliwa na Center for Global Development (CGD) na Repoa.
Alisema kwa siku za hivi karibuni katika bajeti ya serikali zimeongezwa fedha mara dufu kwenye sekta ya elimu, lakini matokeo yamezidi kuwa mabaya tofauti na inavyotarajiwa. “Siyo kila tatizo unatumbukiza fedha…kwa sasa tunatarajia uchumi wa gesi, hivyo ni lazima tuangalie namna ya kuzitumia kwa muundo wa kunufaisha Watanzania wote,” alisema.
Alisema baada ya mahojiano na wananchi wanaoshiriki mkutano huo kabla ya utafiti, amebaini wana uelewa mkubwa na wengi wamekuwa na maoni tofauti juu ya matumizi ya fedha za mapato na matumizi ya gesi pamoja na mafuta na kwamba baadhi wanatamani zitumike kutatua matatizo yaliyopo kwenye maeneo yao.
“Wananchi ndiyo wenye ufahamu mkubwa wa matatizo yao ambayo wangependa serikali iyape kipaumbele mara itakapopata fedha zitokanazo na uchumi wa gesi na mafuta,” alisema.
Alisema kwa sasa serikali inajipanga kikamilifu kabla ya kuingia kwenye uchumi huo kuwa na wataalamu wengi wenye uelewa wa kutosha wa sekta hizo ili kuhakikisha Tanzania inanufaika.

CHANZO: NIPASHE

No comments: