Waziri wa Habari Utamaduni Vijana na Michezo, Dk Fenella Mukangara
akimsikiliza Rais wa tamasha la kimataifa la Lugha na Utamaduni, Ali
Akkiz.
Tanzania itakuwa mwenyeji wa Tamasha la
Kimataifa la Lugha na Utamaduni litakaloandaliwa na Shirika la
Kilimanjaro Dialogue Institute kuanzia tarehe 21-22 Machi 2015. Tamasha hili litafanyika katika Ukumbi wa Mwalimu J.K. Nyerere jijini Dar es Salaam.
Rais wa Shirika la Kilimanjaro Dialogue Institute
Ali Akkiz aliueleza uongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni , Michezo na
Vijana ulioongozwa na Mhe Dr Fenella Mukangara, jinsi walivyojiandaa
kufanikisha tamasha hilo.
Ali Akkiz alifafanua kuwa wawakilishi 18 kutoka
nchi mbalimbali duniani watahudhuria tamasha hilo. Nchi hizo ni pamoja
na Tunisia, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Romania, Nigeria, Kenya, Kongo
(DRC), Afrika Kusini, Iraq, Uganda, Mozambique na Thailand.
Katika kikao kilichofanyika Makao Makuu ya Wizara,
viongozi waliohudhuria kikao hicho ni Waziri Dr Fenella Mukangara,
Naibu Katibu Mkuu Prof Elisante Ole Gabriel na Mkurugenzi Msaidizi wa
Utamaduni Bi Lilliy Beleko.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment