
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete
Mambo yanayoendelea kufanyika nchini hivi sasa
wakati wananchi wakitakiwa kujielekeza katika masuala muhimu yanayohusu
mustakabali wa Taifa letu yanaweza kufananishwa na maigizo kama siyo
sarakasi.
Katika historia ya nchi yetu, hakuna wakati ambapo wananchi walijikuta wakitakiwa kutekeleza majukumu makubwa ya kitaifa kwa wakati mmoja kama ilivyo mwaka huu. Bahati nzuri wananchi wanatambua kwamba majukumu hayo ni mazito na muhimu, hivyo yanahitaji umakini mkubwa katika utekelezaji wake.
Katika historia ya nchi yetu, hakuna wakati ambapo wananchi walijikuta wakitakiwa kutekeleza majukumu makubwa ya kitaifa kwa wakati mmoja kama ilivyo mwaka huu. Bahati nzuri wananchi wanatambua kwamba majukumu hayo ni mazito na muhimu, hivyo yanahitaji umakini mkubwa katika utekelezaji wake.
Tutakuwa hatujakosea tukisema kwamba majukumu hayo
yanayowakabili wananchi mwaka huu ni ya kihistoria, kwani wanapaswa
kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapigakura ili waweze kupiga
Kura ya Maoni kuhusu Katiba Inayopendekezwa Aprili 30 na pia kupiga kura
katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, mwaka huu. Wananchi
wanatakiwa kusoma Katiba Inayopendekezwa kwa umakini mkubwa ili waweze
kufahamu maudhui yake kabla ya kuipitisha au kuikataa katika kura hiyo
ya maoni.
Sheria ya Kura ya Maoni inataka elimu ya uraia
kuhusu Katiba Inayopendekezwa itolewe kwa siku 60 na kampeni za kuunga
mkono au kukataa Katiba hiyo zifanyike kwa siku 30 kabla ya kura hiyo ya
maoni. Ni wazi kwamba muda uliobaki hautoshi kukidhi matakwa ya Sheria
ya Kura ya Maoni, huku uandikishaji wa wapigakura kwa kutumia mashine za
kielektroniki za BVR ukiwa unasuasua sana kutokana na matatizo
mbalimbali. Mpaka sasa uandikishaji unaendelea katika mkoa mmoja tu wa
Njombe, huku mikoa mingine 29 nchini ikiwa inasubiri kuanza kwa kazi
hiyo. Serikali imesisitiza kwamba kazi hiyo itamalizika katika muda
uliopangwa, ingawa wananchi wengi siyo tu wamepoteza matumaini ya
kufanyika kwa Kura ya Maoni katika muda uliobaki, bali pia wanaona
utakuwa muujiza wa kipekee kazi hiyo kumalizika kwa muda katika
mazingira kama hayo.
Hofu ya wananchi wengi ni kwamba siasa imegubika
masuala hayo kwa kiasi kikubwa na kusababisha viongozi kutoa kauli
tatanishi zisizoendana na hali halisi, huku wananchi wakiwa hawaoni
utekelezaji wa masuala hayo kama Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na
Sheria ya Kura ya Maoni zinavyoelekeza. Kwa mfano, pamoja na mchakato wa
kupata Katiba Mpya kuanza miaka minne hivi iliyopita, wananchi
wameshuhudia porojo kuliko vitendo kwa upande wa viongozi na wanasiasa.
Ndio maana inashangaza kuona kwamba Serikali imeipatia Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC), mashine za BVR 250 tu badala ya mashine zaidi ya 8,000
zinazohitajika kuandikisha wapigakura nchi nzima.
Kama tulivyosema awali, kinachoendelea mpaka sasa
ni kama maigizo au sarakasi. Masilahi ya Taifa yamewekwa kando na baadhi
ya watu wamechukulia mchakato wa kupata Katiba Mpya na kuelekea
Uchaguzi Mkuu kama fursa ya kutimiza ndoto zao. Wananchi wanajiuliza:
Imekuwaje Serikali ishindwe kupata fedha za kununua mashine 8,000 za
BRV, badala yake ifuje fedha ikizunguka katika nchi mbalimbali, ikiwa ni
pamoja na Kenya na Nigeria kuazima mashine za BVR bila mafanikio? Nini
hiyo kama sio aibu iliyopitiliza kwa Taifa letu kwa kufanya mzaha kwa
mambo nyeti kwa mustakabali wa Taifa letu kama kupata Katiba Mpya na
kufanya Uchaguzi Mkuu?
Imebaki miezi saba tu kufanya Uchaguzi Mkuu. Kwa
mwendo huu wa uandikishaji wa wapigakura, nani anasema muda huo
utatosha? Nani anasema muda uliobaki kabla ya kupiga Kura ya Maoni
unatosha?
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment