Kanal Mamadou Ndala anayedaiwa kuuawa na njama za Kanal Birocho Nzanzu
Mahakama
ya kijeshi Mashariki mwa Jamuhuri ya Demokrasi ya Congo imemhukumu kifo
Kanali Birocho Nzanzu baada ya kubainika na makosa ya kutaka kumuua
afisa wa jeshi la nchi hiyo aliyekuwa mstari wa mbele kutokomeza
wapiganaji wa M23.
Afisa anayedaiwa kupangiwa njama za kuuawa ni Mamadou Ndala mabaye kwa kiasi kikubwa aliamini katika vita dhidi ya kundi hilo la wapiganaji na ambaye aliuawa mwezi januari mwaka huu. Hata hivyo hukumu hiyo imetolewa kwa watuhumiwa nane ambapo kati ya hao mmoja ndiye Kanali Ndala aliyehukumiwa kifo. Mahakama imebainisha kuwa Kanali Nzanzu amekuwa akitumiwa na waasi wa ADF kutoka Uganda kuandaa maujaji.
CHANZO: BBC SWAHILI
Afisa anayedaiwa kupangiwa njama za kuuawa ni Mamadou Ndala mabaye kwa kiasi kikubwa aliamini katika vita dhidi ya kundi hilo la wapiganaji na ambaye aliuawa mwezi januari mwaka huu. Hata hivyo hukumu hiyo imetolewa kwa watuhumiwa nane ambapo kati ya hao mmoja ndiye Kanali Ndala aliyehukumiwa kifo. Mahakama imebainisha kuwa Kanali Nzanzu amekuwa akitumiwa na waasi wa ADF kutoka Uganda kuandaa maujaji.
CHANZO: BBC SWAHILI

No comments:
Post a Comment