Naibu Waziri Wizara ya Fedha, 
Adam Malima ametoa siku 14 kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kukaa na
 wafanyabiashara nchini na kutatua kero zote za kodi zilizopo.
                
              
Alisema hayo katika kikao cha Kamati ya Bunge ya 
Uchumi, Viwanda na Biashara kilichowataka wafanyabiashara kueleza kero 
zao na Kamishna wa TRA kuzijibu. Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao, Johnson Minja 
alilalamikia kutokuwapo kwa uwazi katika ulipaji kodi na utapeli uliopo 
miongoni mwa kampuni za kutoa na kupokea mizigo.
Alisema wakiagiza kontena la mzigo, ushuru wa TRA 
unaweza kulipa Sh100 milioni huku kwa mawakala wa kutoa na kupokea 
mizigo ukitoa Sh40 milioni lakini unapewa risiti ya Sh12 milioni. Minja aliomba uwepo mfumo wa ulipaji kodi 
unaoonyesha gharama halisi za mzigo husika na siyo mfumo wa sasa 
unaowaumiza na uliojaa rushwa.
Mbunge wa Ziwani, Ahmed Ngwali ambaye ni mjumbe wa
 kamati hiyo alisema, kutokana na kuwapo kwa rushwa iliyokithiri TRA 
haina sababu ya Kamishna, Rished Bade kuendelea kuwapo kwenye taasisi 
hiyo.
Ngwali alisema, Bade alikuwa akikaimu nafasi hiyo 
na sasa ni kamishna kamili hivyo angeweza kumaliza tatizo la rushwa TRA,
 lakini ameshangazwa na ongezeko la vitendo hivyo.
Alibainisha kuwa, fedha walizotegemea ziende kwenye miundombinu na afya sasa zinaenda kwenye mifuko ya watu. Kuhusu na mfanyabiashara wa Home Shopping Centre, 
Mbunge wa Konde, Khatibu Said alihoji kwa nini anahodhi zaidi ya 
asilimia 90 ya makontena bandarini na hakuna ripoti ya taarifa yoyote 
kuhusu hilo licha ya kamati kuiomba.
Akijibu tuhuma hizo, Kamishna Bade alisema, suala 
hilo alikwishalisikia na wanafanya kila njia kuwakamata lakini peke yake
 hawezi, lazima washirikiane. Mwenyekiti wa kamati hiyo, Luaga Mpina alisema ni 
lazima Watanzania wote walipe kodi na wapo tayari kugombana na wakwepa 
kodi, kwani nchi zote zilizoendelea zilikusanya kodi.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment