Baada ya kuona makala zilizoeleza sababu 
mbalimbali zinazosababisha matatizo ya nguvu za kiume, sasa tuwe pamoja 
kwa nguvu zote katika kipengele muhimu kinachohusu suluhisho la matatizo
 ya nguvu za kiume.
Kikubwa unachotakiwa kufanya ili kuweza kupata msaada wa tatizo hili ni kuwa tayari kuweka wazi tatizo lako kwa watoa huduma za afya wa tiba za binadamu, na sio kwa watoa huduma wasiotambulika. Uzoefu unaonyesha wanaume wengi wenye tatizo hili huenda kwa watu wababaishaji wanaofanya ujanja ili kupata fedha.
Kikubwa unachotakiwa kufanya ili kuweza kupata msaada wa tatizo hili ni kuwa tayari kuweka wazi tatizo lako kwa watoa huduma za afya wa tiba za binadamu, na sio kwa watoa huduma wasiotambulika. Uzoefu unaonyesha wanaume wengi wenye tatizo hili huenda kwa watu wababaishaji wanaofanya ujanja ili kupata fedha.
Ikumbukwe kuwa kuficha tatizo lako na kuendelea 
kusikiliza maneno ya vijiweni kwa marafiki ambao hawana uelewa na mambo 
haya kunazidi kukuchanganya na kukuchelewesha katika kupata matibabu 
sahihi, sehemu sahihi na kwa wakati muafaka. Ni vyema kutokurupuka na 
kuhangaika kwa matabibu ambao ni matapeli wanaotaka kutumia matatizo 
yako ya nguvu za kiume kama mtaji wao wa kujipatia fedha.
Wagonjwa wengi huwa na aibu kufika katika huduma 
za afya kwa ajili ya uchunguzi wa tatizo hilo wakihofia kunyanyapaliwa, 
lakini jambo hilo halipo kwa wataalamu wenye taaluma ya tiba za 
binadamu. Kumbuka kuwa si wewe pekee uliye na tatizo hilo, ni mamilioni 
ya watu duniani kote wana tatizo hilo hivyo unatakiwa kujiamini na 
kujipa moyo kuwa tatizo hili linatatulika.
Hata kama ikitokea kuwa tatizo lako linaweza 
lisitatulike ni vizuri ukakubaliana na hali hiyo, tambua kuwa kukosa 
nguvu za kiume si mwisho wa maisha yako. Kuna mambo ya maana na mazuri 
kwa maendeleo ya maisha yako ya baadaye unayoweza kuyafanya ili kusukuma
 maisha yako.
Kuwapo kwa matangazo mengi mtaani ya dawa za 
kuongeza nguvu za kiume hakumaanishi kuwa zinaweza kutatua tatizo lako, 
hiyo ni biashara ya wajanja mitaani.
Unaweza ukawa unatumia dawa hizo na kupata nafuu na kudhani umepona, lakini kumbe ukawa unaudhuru mwili wako pasipo kujua.
Dawa hizo zisizothibitishwa wala kupendekezwa kama
 ni salama na Taasisi ya Chakula na Dawa (TFDA), zipo kila mahali 
mitaani na wengi hujikuta wakinunua na kuzitumia kiholela. Tayari imeishawahi kuripotiwa kupoteza maisha 
baada ya kunywa dawa hizo kiholela pasipo kuzingatia ushauri wa 
wataalamu wa tiba za binadamu.
Miaka ya nyuma tatizo hili lilikuwa linaonekana 
kujitokeza zaidi kwa wanaume wenye umri kati ya miaka 40 na kuendelea. 
Lakini katika miaka ya siku hizi hata vijana wa kati ya umri wa miaka 20
 na 30 wanajikuta wanapatwa na tatizo hilo. Tatizo la nguvu za kiume linaweza kutibiwa au likapunguzwa makali kwa matibabu mbalimbali baada ya kufanyiwa uchunguzi yakinifu.
Yapo matatizo ya nguvu ya kiume ambayo hujikuta 
hayatatuliki kwa njia yoyote hivyo mtu mwenye tatizo hilo huwa ni 
ulemavu wa kudumu. Kabla ya kufika huko ni vizuri ukatambua kuwa yapo matibabu 
salama ambayo unaweza kuyafanya kuimarisha hali ya tendo kabla ya 
kumfikia daktari.
                
              
Mazoezi ni moja ya kitu muhimu kwa mtu mwenye 
tatizo hili kwani humsaidia mtu kuwa imara na kuwa na ufanisi kwa mwili 
wake. Yawezekana umekua mtu mzima lakini kufanya mazoezi mepesi ya 
kutembea yanasaidia. Unene uliopitiliza na mrundikano wa mafuta mwilini 
huweza kupunguza ufanisi wa homoni ya kiume. Homoni ya kiume ndio 
inahusika kwa wanaume kuweza kuwa na nguvu hizo.
Unene ndio chanzo cha kupata maradhi ikiwamo 
kisukari, magonjwa ya moyo, mishipa ya damu na shinikizo la damu. 
Maradhi haya ndio yanayoharibu mishipa ya damu na mishipa ya fahamu ndio
 chanzo kikuu cha kupungukiwa nguvu za kiume.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment