Wenyekiti wa UKAWA Freeman Mbowe (CHADEMA), Profesa Ibahimu Lipumba (CUF) na James Mbati (NCCR-Mageuzi). Hakuna ambaye alitarajia uchaguzi wa Serikali za Mitaa na vijiji mwaka huu kama ungekuwa na upinzani mkubwa kama uliotokea.
Tumeshuhudia katika uchaguzi huu, watu wakipigana
hadi damu kumwagika, nyumba kuchomwa moto, masanduku ya kura kuibwa na
kura kuchomwa moto na hata kukamatwa kwa baadhi ya wabunge na wanasiasa. Uchaguzi huo uliofanyika kuanzia Desemba 14, mwaka
huu, licha ya kuwa na upungufu mkubwa uliosababisha kurejewa katika
maeneo kadhaa, lakini umetoa funzo kubwa kwa Watanzania na hasa vyama
vya kisiasa.
Uchaguzi wa mwaka huu, tofauti na chaguzi
zilizopita, umewaweka matatani wakurugenzi wa halmashauri 17, sita kati
yao wakifukuzwa kazi, watano wakipewa onyo na wengine sita
wakisimamishwa. Jingine kubwa, katika uchaguzi huu, ulikuwa ni
muungano wa vyama vya upinzani, kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi
(Ukawa) kuamua kusimamisha mgombea mmoja katika nafasi mbali mbali.
Katika chaguzi zote zilizopita tangu kuanza mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, hakukuwahi kuwa na muungano kama huu. Ingawa mara kadhaa, viongozi wa upinzani walikuwa
wakikutana na kukubaliana kuungana na kusimamisha mgombea mmoja katika
nafasi mbali mbali, lakini wamekuwa wakivurugana.
Safari hii, Katika uchaguzi wa Serikali za mitaa,
walau baadhi ya vyama vinavyounda Ukawa walikubaliana kusimamisha
mgombea mmoja katika maeneo kadhaa nchini. Licha ya mpango huu, pia kukabiliwa na vikwazo
kidogo, lakini kwa kiasi kikubwa umeweza kuvinufaisha vyama vya upinzani
kwa kuwaunganisha wanachama wao kupambana na wana CCM katika kura.
Vyama ambavyo viliungana kupitia ukawa ni Chadema, CUF, NLD na NCCR- Mageuzi. Muungano huu umesababisha matokeo tofauti kubwa ya matokeo ikilinganishwa na ule wa mwaka 2009. Takwimu zinasoma wakati mwaka 2009 CCM ilishinda
vijiji 9,800, mwaka huu imeshinda vijiji 7,290 licha ya vijiji kadhaa
kuongezwa katika maeneo mengi nchini.
Kwa upande wa Serikali za mitaa, CCM mwaka 2009 ilishinda
vitongoji 2,242 lakini safari hii, imeanguka kwa kushinda vitongoji
2,116 tu licha ya vitongoji vipya vingi kuongezwa.
Upinzani kwa ujumla imefanya vizuri kwa kuongeza
viti, kwa vyama vya Chadema na CUF, wakati chadema mwaka 2009 walikuwa
na uongozi wa vijiji 289 mwaka huu, wameshinda na kupata viti 1,248.
upande wa vitongiji walikuwa na 124 na sasa wameshinda 753.
Chama cha Wananchi CUF walikuwa na viti 407 vya
vijiji, mwaka 2009 lakini sasa wanaviti 945 wakati walikuwa na vitongoji
133 lakini sasa wanavitongoji 235 .
Matokeo haya ni kabla ya marejeo ya uchaguzi uliofanyika Desemba 21, katika maeneo mbali mbali nchini.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John
Mnyika na Naibu Mkurugenzi wa habari na Uenezi-CUF, Abdul Kambaya,
wajumbe wa sekretarieti ya Ukawa, wamezungumza na gazeti hili kwa
nyakati tofauti na kueleza siri ya mafanikio yao katika uchaguzi huo wa
Serikali za Mitaa. Wote kwa pamoja wanatoa sababu zinazofikia 10
ambazo wanaamini ndizo zimechangia ushindi wao kama Ukawa katika
uchaguzi huo na kuzitaja.
Ziara za mikoa na operesheni mbali mbali.
Mnyika anasema tofauti na miaka ya nyuma, vyama
vya upinzani vilikuwa vikitupiwa lawama kuwa ni vyama vya uchaguzi kwani
baada ya chaguzi kwisha hupotea lakini tangu uchaguzi wa mwaka 2010
hali imebadilika.
Anasema safari hii baada ya uchaguzi wa mwaka
2010, vyama vya upinzani hasa Chadema, hawakulala waliendelea na
mikutano mikoani na operesheni mbali mbali ambazo zilikwenda sambamba na
kutolewa elimu ya uraia, “tulikuwa na operesheni Sangara, tukaja vuguvugu
la mabadiliko, Delete CCM kabisa na nyingine nyingi ambazo zimesaidia
kufikisha ujumbe hadi vijijini,” anasema
Chadema ni msingi.
Mnyika anasema katika maeneo mengi nchini, kupitia
mikutano ya chini kwenye matawi waliibua kampeni ya Chadema ndio
msingi, kutokana na mikutano iliyofanyika vijijini. Anasema mpango huu ulisaidia sana kukijenga chama hicho vijijini
tofauti na miaka ya nyuma kwani vikao vilifanyika kutathimini
mabadiliko.
Muungano wa UKAWA.
Mchakato wa katiba mpya.
Sakata la Escrow.
Kero za wananchi
Wagombea wanaokubalika.
Vyombo vya habari.
CHANZO: MWANANCHI
Anasema katika mpango huo, walikubaliana kuwa na
mtandao wa upinzani vijiji hadi kuwa na mabalozi jambo ambalo
limefanikiwa sana.
Muungano wa UKAWA.
Abdul Kambaya na Mnyika wanasema muungano wa Ukawa
umekuwa na mafanikio makubwa, kwani awali walikuwa na migongano wakati
wa kupitisha wagombea lakini safari hii wamekubaliana.
Kambaya anasema ingawa baadhi ya maeneo viongozi
wa ngazi za chini walishindwa kufikia maridhiano ya kusimamisha mgombea
mmoja, lakini kwa maeneo mengi wagombea wamesimamishwa na hivyo wananchi
kuwa na imani na Ukawa na kuwapa ushindi.
Mchakato wa katiba mpya.
Viongozi hawa wa Chadema na CUF, kila mmoja
anasema mchakato wa Katiba Mpya na msimamo wa Ukawa kutetea maoni ya
wananchi umekuwa na manufaa makubwa kwao.
Kambaya anasema wananchi wameelewa dhamira ya
dhati ya Ukawa kuhakikisha taifa linakuwa na Katiba ambayo inatokana na
maoni yao na siyo maoni ya CCM. Kwa upande wake Mnyika anasema, suala la katiba
limewanufaisha kwani wananchi wameamini kuwa Ukawa ndiyo tegemeo lao kwa
sasa baada ya kutoa maoni yao lakini CCM wamepinga.
Vita dhidi ya ufisadi na utetezi wa rasilimali.
Mnyika anasema, vita dhidi ya ufisadi iliyoanza
mwaka 2005 pale Dk Wilbroad Slaa alipotangaza orodha ya mafisadi
imeendelea hadi sasa “kuanzia bungeni hadi kwenye mikutano yetu
tumekuwa tukiibua ufisadi na kusimamia wachukuliwe hatua wahusika jambo
ambalo limesaidia sana kuwaonyesha wananchi nini malengo yetu,” anasema, “michango yetu kutaka rasilimali za nchi kunufaisha
Watanzania kama madini, mafuta, ardhi, gesi na mengine mengi imekuwa
siri kubwa ya ushindi wetu.”
Sakata la Escrow.
Kambaya anasema sakata la wizi wa zaidi ya Sh306
bilioni katika akauti ya Tegeta Escrow, limeongeza mori ya wananchi
kuwaunga mkono Ukawa. Kambaya anasema suala hili ingawa Serikali ya CCM
inalipuuza lakini limeibua dhana kubwa ya kutaka uwajibikaji kwa
wahusika kama Ukawa unavyotaka. “suala hili limetunufaisha sana Ukawa kwani
wananchi sasa wamechoshwa na ufisadi unaofanywa na watendaji wa Serikali
ya CCM,” anasema.
Kero za wananchi
Mnyika anasema kukithiri kwa Kero za wananchi
vijijini kama uhaba wa maji, huduma za afya, umasikini, matatizo ya
elimu yamewafanya kuichoka CCM. Anasema viongozi wa CCM wamekuwa wakiahidi mambo
mengi lakini wameshindwa kuyatekeleza hasa yale ambayo yanagusa wananchi
masikini. Mnyika anasema CCM kutotimiza ahadi zao,
kumewafanya wananchi kutowaamini wagombea wao hadi ngazi za chini na
hivyo, kuwapigia kura Ukawa.
Wagombea wanaokubalika.
Mnyika anasema katika maeneo mengi wagombea waliotokana na Ukawa walikuwa wanakubalika baada ya kupitia michujo mingi. “Kwa mfano sisi Chadema tulikuwa na wagombea, CUF
walikuwepo na NCCR- Mageuzi lakini kutokana na kukubaliana kuwa na
mgombea mmoja, walichujwa hadi kupatikana mmoja anayekubalika,” anasema. Anasema mchujo huo, ulisababisha maeneo mengi Ukawa kuwa na
wagombea ambao ni chaguo la wananchi, ingawa wengi waliwekewa
mapingamizi na kuondolewa.
Vyombo vya habari.
Kambaya anasema ushindi wa Ukawa hauwezi kuvitenga
vyombo vya habari kutokana na kuibua kwa kutangaza mambo mengi ambayo
ni kero katika jamii bila woga yaliyokuwa yakiibuliwa na viongozi wa
vyama vinavyotokana na Ukawa. Anasema pia vyombo vya habari tangu kutangazwa
muungano wa Ukawa, vimeonyesha kuwaunga mkono kwa kutetea umoja na
kupingana kutengana. “kwa niaba ya Ukawa tunavishukuru sana vyombo vya
habari kwa kuwa mstari wa mbele kwanza kufichua maovu katika jamii na
pia kukemea kutengana Ukawa wakati wote,” anasema Kambaya. Anasema kufafanuliwa kwa kashfa nyingi ambazo
zinatafuna fedha za umma kama sakata la wizi wa fedha za Escrow
kumefanya wananchi kuwa na imani na upinzani kama watetezi wao. Hata hivyo, viongozi hawa kwa pamoja wanakiri kuwa ushindi wa Ukawa haukuwa rahisi katika uchaguzi huu.
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment