Social Icons

Pages

Thursday, December 04, 2014

JAJI MKUU ATAKA UWAZI MAHAKAMANI

Jaji Mkuu, Chade Othman akimsikiliza Rais wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Jaji Thomas Mihayo (kushoto) baada ya kufungua mkutano wa wa majaji na wahariri wa vyombo habari Dar es Salaam jana. Wa pili kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Biashara, Robert Makaramba na Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga.


Jaji Mkuu Chande Othman ametaka mahakama ziruhusu waandishi wa habari kupata taarifa za yanayoendelea mahakamani ili kupata taarifa sahihi.
“Umefika wakati Mahakama kuondoa sababu zisizo za msingi za kuzuia wanahabari kupata taarifa za mambo yanayoendelea mahakamani,” alisema Jaji Othman wakati wa mkutano wa majaji na wahariri wakuu uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo, alionya kuwa “wanahabari wanapaswa kuwasiliana na mahakama ili kuipa nafasi ya kujitetea pale inapoingizwa katika tuhuma.”
Alisema mkutano huo ni sehemu muhimu ya kumaliza matatizo ambayo yamekuwa chanzo cha malalamiko dhidi ya vyombo vya habari, kutokana na mahakama kujifungia katika chumba na kutotoa taarifa sahihi kwa wakati pale zinapohitajika.
Alisema wanahabari wanatakiwa kuandika ukweli kwa kufuata maadili yao na waipe mahakama nafasi ya kujitetea.
Alisema kusiwe na ugumu katika utendaji wa mahakama na wanahabari ili kila mtu afanye kazi kwa uhakika na kuheshimu uhuru, maadili na haki ya demokrasia ya kupata habari inayotolewa na Katiba.
Alisema vyombo vya habari na mahakama ni nyenzo muhimu katika kukuza utawala wa sheria na demokrasia, hivyo ushirikiano baina ya mihimili hiyo unahitaji mtazamo mpya.
Alisema mihimili hiyo ni kimbilio la wananchi katika kipindi hiki ambacho demokrasia ya kweli ‘inakata mizizi’ yake, hivyo kuhitaji ushirikiano wa kipekee. Mwenyekiti wa Baraza la Habari (MCT), Jaji Joseph Mihayo alisema Mahakama itende haki ili kurahisisha upatikanaji wa habari.
kwa kutoa fursa kwa wananchi kupata taarifa sahihi kwa wakati kuhusu kile kinachojiri mahakamani.

CHANZO: MWANANCHI

No comments: