Katika barua yake kwa Rais Jakaya Kikwete, Jaji 
Werema alisema ameomba kujiuzulu kwa sababu; “ushauri wake kuhusiana na 
suala la Escrow hakueleweka na umechafua hali ya hewa.”
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu
 ilisema jana kuwa Rais Kikwete amekubali ombi hilo la kujiuzulu na 
amemshukuru Jaji Werema kwa; “utumishi wake ulioongozwa na uaminifu na 
uadilifu.”
Jaji Werema ambaye mara kwa mara amekuwa akitetea 
ushauri katika sakata hilo, amechukua uamuzi huo katika siku ya mwisho 
ya wiki moja iliyoahidiwa na Rais Kikwete kukamilisha uchambuzi wa 
taarifa za Bunge na kutoa uamuzi dhidi ya wahusika wa sakata hilo.
Uamuzi wa Werema unatokana na mazimio ya Bunge ya 
kutaka yeye na baadhi ya vigogo wachukuliwe hatua kutokana na madai ya 
kuhusika kwenye sakata la uchotwaji fedha katika akaunti hiyo.
Mwanasheria huyo alilalamikia maazimio hayo 
akisema hayakuwa ya haki kwa wote waliotuhumiwa na uamuzi huo ulifanywa 
kwa hasira na kufuata mkumbo.
Bunge liliazimia Jaji Werema kushughulikiwa kwa 
mujibu wa sheria kutokana na kuipotosha Serikali kuhusu malipo ya Sh306 
bilioni kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow, akishauri fedha hizo zilipwe 
kwa Kampuni ya IPTL iliyo na mkataba wa ufuaji umeme na Tanesco bila ya 
kukata kodi.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment