
Naibu Waziri wa Ardhi, George Simbachawene.
Naibu Waziri wa Ardhi, George Simbachawene alitoa
agizo hilo juzi alipozungumza na wananchi wa Kijiji cha Valesca ambao
wiki iliyopita walivamia shamba hilo na kugawana.
Alisema hekali 1,500 za shamba hilo zilizotolewa na ACU ili zigawanywe, ni lazima zipimwe ili wanaohitaji ardhi wapewe.
Alisema kuna wanaomiliki eneo kubwa la ardhi ndani
ya Shamba la ACU, hivyo ni lazima taratibu zifuatwe ili wapunguziwe na
wengine wanufaike.
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari aliunga mkono uamuzi huo kwa kuwa maelfu ya wananchi wa eneo hilo hawana ardhi.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment