Naibu Spika, Job Ndugai
ambaye alipotea bungeni wakati wa mjadala moto wa sakata la akaunti ya
Tegeta Escrow na kuzua maswali mengi, jana ameibukia katika sakata la
wafanyabiashara baada ya wabunge kuwasha moto kutaka Serikali isikilize
madai yao na kumwachia mwenyekiti wa jumuiya yao, Johnson Minja
aliyenyimwa dhamana.
Ndugai alipotea katikati ya mkutano wa kumi na sita na kumi na saba wa Bunge uliojadili Escrow na jana aliibuka na kuongoza kikao cha Bunge kilichokuwa na mjadala mkali wa mgomo wa wafanyabiashara baada ya wabunge bila kujali itikadi zao kuibana Serikali wakiitaka ifanye kila njia kumwachia kwa dhamana Mwenyekiti wa Wafanyabiashara nchini, Johnson Minja kwa maelezo kuwa ikifanya hivyo itatuliza migomo hiyo. Kutokana na hali hiyo, Ndugai alilazimika kuiomba Kamati ya Uongozi ikutane, kujadili suala hilo na kutoa ushauri kwa Serikali.
Ndugai alipotea katikati ya mkutano wa kumi na sita na kumi na saba wa Bunge uliojadili Escrow na jana aliibuka na kuongoza kikao cha Bunge kilichokuwa na mjadala mkali wa mgomo wa wafanyabiashara baada ya wabunge bila kujali itikadi zao kuibana Serikali wakiitaka ifanye kila njia kumwachia kwa dhamana Mwenyekiti wa Wafanyabiashara nchini, Johnson Minja kwa maelezo kuwa ikifanya hivyo itatuliza migomo hiyo. Kutokana na hali hiyo, Ndugai alilazimika kuiomba Kamati ya Uongozi ikutane, kujadili suala hilo na kutoa ushauri kwa Serikali.
Kabla ya kuahirisha Bunge jana mchana, Ndugai
aliwaeleza wabunge kuwa kamati hiyo imeitaka Serikali kuharakisha
mazungumzo yake na wafanyabiashara ili kumaliza malalamiko yao ambayo
ni; ongezeko la kodi kwa asilimia 100, matumizi ya mashine za
kielektroniki (EFD’s) na Minja kuachiwa kwa dhamana.
Mjadala mkali uliibuka baada ya kipindi cha
maswali na majibu, baada ya wabunge 10 kusimama na kutaka kuomba
mwongozo wa Spika wakishinikiza mgomo huo ujadiliwe kwa dharura kwa
maelezo kuwa, unasababisha Serikali kukosa mapato na kuwatesa wananchi
wanaohitaji kupata huduma.
Mbunge wa kwanza kupewa ruhusa ya kuzungumza
alikuwa ni Deo Sanga (Njombe Kaskazini-CCM), aliyetaka kujua sababu za
Serikali kutotoa majibu ya uhakika wakati ikijua wazi kuwa mikoa ya
Mbeya, Arusha, Dodoma na Tabora kulikuwa na migomo ya kimya kimya.
Kauli hiyo iliungwa mkono na Mbunge wa Tabora
Mjini (CCM), Ismail Aden Rage akisema kuwa Tabora mjini maduka
yamefungwa tangu juzi na wananchi wanahangaika kwa kukosa huduma.
Alipopewa nafasi Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima
Mdee alitaka Bunge lijadili mgomo huo kwa dharura kwa kuwa hali ni mbaya
nchini.
Akitoa ufafanuzi wa Serikali, Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Jenister Mhagama alieleza
kuwa Serikali inafanya mazungumzo na wafanyabiasha na yapo katika hatua
nzuri, kuhusu ongezeko la kodi na matumizi ya mashine za EFD’s.
Kauli hiyo iliungwa mkono na wabunge wa CCM,
akiwemo Rage na Sanga waliotaka wabunge wenzao wakubaliane na kauli ya
Serikali na kuipa muda lakini wabunge wa upinzani walipinga.
Pia maelezo hayo ya Serikali yalipingwa na
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara, Luaga
Mpina akisema kuwa tangu tume ya maridhiano kuundwa Julai mwaka jana,
Serikali haijaitisha kikao na wafanyabiashara hao.
Alisema baada ya kamati hiyo kushinikiza hatimaye
Serikali ilikubali kufanya hivyo kukutana na wafanyabiashara hao Ijumaa
iliyopita, kwamba kati ya makubaliano hayo ni pamoja na Minja kuachiwa
huru.
“Inashangaza kuona kwamba pamoja na mazungumzo ya kina, Serikali
imeshindwa kusimamia na kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa,” alisema.
Mvutano huo ulimuinua Mwanasheria Mkuu wa
Serikali(AG), George Masaju na kuwataka wabunge waende mahakamani kwa
ajili ya kutoa hoja za kumtoa Minja kwa dhamana na si bungeni kauli
ambayo ilimfanya azomewe na baadhi ya wabunge.
“Minja aliachiwa kwa dhamana lakini alikiuka
masharti ya dhamana kwa kuitisha vikao na migomo. Hapo ndipo Serikali
ilipoieleza mahakama ambayo ilimfutia dhamana,” alisema Masaju.
Kauli hiyo ya Masaju iliwakera wabunge wengi huku
Mbunge wa Mbozi Magharibi (Chadema), David Silinde akishangazwa na
Serikali kuendelea kumshikilia kiongozi huyo wakati hajatenda kosa la
kufanya anyimwe dhamana.
Baada ya hali ya hewa kuchafuka zaidi, Ndugai ndipo alipotoa agizo la Kamati ya Uongozi kukutana ili kupata majibu ya uhakika.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment