Social Icons

Pages

Wednesday, April 01, 2015

JUKWAA LA WAKRISTO: JUNA LETU LISITUMIKE VIBAYA

Rais Jakaya Kikwete.
Jukwaa la Wakristo Tanzania, limesema linashangazwa na tabia ya baadhi ya viongozi wa serikali wenye tabia ya kuitisha mikutano wanayoiita ni ya viongozi wa dini huku ikiwa siyo rasmi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Jukwaa hilo, imeeleza kuwa viongozi hao wamekuwa chanzo cha mvutano uliopo baina ya dini mbili na kwamba watakuwa chanzo cha kuvurugika kwa amani nchini.
Taarifa hiyo ambayo imesainiwa na Mkuu Habari na Mawasiliano wa Baraza la Kikiristo Tanzania (CCT), Mchungaji John Kamoyo, ilisema jopo la Maaskofu kutoka TEC, CPT lilikutana Machi 30, mwaka huu, mjini Dodoma, kuondoa dhana kuwa linaongozwa na hasira na mihemko katika kufikia maamuzi linavyoyafanya kama wengine wanavyotafsiri bali linasukumwa kwa upendo wa wananchi ili kujenga taifa lenye umoja, amani, utulivu na maelewano.
Kamoyo alisema Machi 03, 2015 Waziri Mkuu aliitisha mkutano kupitia Mchungaji mmoja ambapo hakuna kiongozi wa taasisi au Kanisa aliyeshiriki, na kwamba Machi 28, mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete, alikutana na kikundi ambacho sio rasmi yaani Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es Salaam.
“Maaskofu tuliokutana Dodoma hatuongozwi na hasaira wala mihemko katika kufanya uamuzi kama wengine wananavyotafsiri, tunafikia uamuzi baada ya maombi kwa upendo wa wananchi na kujenga taifa lenye umoja na amani,” alisema Mchungaji Kamoyo.
Kamoyo alisema walikewenda Dodoma kufuatilia kwa kina Muswada wa Sheria mbalimabali za mwaka 2014 pamoja na mrekebisho mengine ya Sheria ya Tamko la Sheria za Kiislamu la mwaka 1964.

CHANZO: NIPASHE

No comments: