Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima akilalamika kwa
maumivu alipokuwa akisaidiwa kuingia kwenye gari la Polisi wakati
akitolewa Hospitali ya TMJ na kupelekwa katika Kituo cha Polisi
Oysterbay Dar es Salaam, jana.
Askofu wa Kanisa
la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ameruhusiwa kutoka hospitalini
alikokuwa amelazwa na baadaye kuachiwa na polisi kwa dhamana isiyokuwa
na masharti.
Gwajima aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya TMJ
alichukuliwa Kituo cha Polisi Oysterbay kwa kuwa jana ndiyo tarehe
aliyokuwa ameitwa kuendelea na mahojiano baada ya kupoteza fahamu akiwa
katika mahojiano ya awali.
Dk Fortunatus Mazigo aliyekuwa akimtibu Gwajima,
alisema anaendelea vizuri hivyo angepewa kibali cha muda kutoka kwa
sababu afya yake haikuwa imeimarika kwani hata kusimama ilikuwa ni
lazima apate msaada.
Muda mfupi kabla ya kuruhusiwa lilifika gari la polisi aina ya Land Cruiser hospitalini hapo likiwa na askari wanne wenye bunduki na baada ya muda, likifuatiwa na gari jingine dogo la polisi aina ya MG6 Turbo.
Muda mfupi kabla ya kuruhusiwa lilifika gari la polisi aina ya Land Cruiser hospitalini hapo likiwa na askari wanne wenye bunduki na baada ya muda, likifuatiwa na gari jingine dogo la polisi aina ya MG6 Turbo.
Polisi walioshuka kwenye gari ndogo walikwenda
wodini alipokuwa amelazwa Askofu Gwajima na baada ya muda walirudi naye
katika lifti.
Akiwa amevaa suti ya rangi ya kijivu na shati
jekundu, Gwajima akiwa kwenye kiti cha magurudumu kilichopelekwa
hospitalini na wasaidizi wake, akionekana mwenye maumivu aliingizwa
katika gari hilo dogo na kupelekwa Kituo cha Polisi Oysterbay.
Alipofika katika mlango wa chumba cha Mkuu wa
Upelelezi wa Kituo hicho, Salum Ngalama, ofisa huyo aliamuru Gwajima
apewe dhamana na kesho aende Kituo Kikuu cha Polisi.
Baada ya kukamilisha taratibu, aliachiwa na
baadaye aliwaambia waandishi wa habari kuwa ifike mahali viongozi wa
dini waheshimiane na wanapokosolewa waache malumbano yasiyo kuwa na
sababu.
Alisema katika jamii iliyostaarabika kuelekezana
na kukemeana pale mmoja anapokosea ni kawaida na iwapo itafikia hatua
hiyo hakuna haja ya mwingine kupiga kelele badala yake ayafanyie kazi
aliyoelekezwa.
“Viongozi wa dini tuheshimiane, tusiwe wakali
tunapokemewa na kuleta malumbano yasiyo ya msingi,” alisema Gwajima na
kuelekea nyumbani kwake.
Njia ya kuelekea kanisani anakotoa huduma askofu
huyo, Kawe jijini Dar es Salaam, kulikuwa na makundi ya watu wakiimba
nyimbo za kusifu, wengine wakiwa wamebeba matawi ya miti, wakitoka
katikati ya Jiji ambao walijiunga na wenzao waliokuwa polisi na kuanza
safari kuelekea Kawe.
Wakili wa Gwajima, John Mallya alisema mteja wake
ameachiwa kwa dhamana bila masharti yoyote na kutakiwa kufika kituo
Kikuu cha Polisi kesho.
CHANZO: MWANANCHI
Alisema wachungaji 15 waliokamatwa kwa tuhuma za kutaka
kumtorosha Askofu huyo wameachiwa pia, ingawa itawalazimu kuhoji
kushikiliwa kwao zaidi na kuwekwa ndani zaidi ya saa 24.
Baadhi ya wachungaji hao walisema kuwa licha ya kukaa ndani siku tatu hawafahamu walikamatwa kwa sababu gani.
Mchungaji Yekonia Biyagaze alisema, hafahamu hadi
leo alikamatwa kwa sababu gani, kwani hakufanya fujo, kutukana, kupiga
kelele bali kumuhudumia mgonjwa. Mchungaji Fredrick Fussi alisema kama wana hatia wapelekwe mahakamani na wapo tayari kujibu tuhuma dhidi yao.
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment