Ndugu Potty Msuku
Serikali ya Qatar inajenga bandari mpya katika eneo la jangwa, mradi unaogharimu Dola za Marekani 80 bilioni na ikimteua raia wa Tanzania asimamie kazi hiyo.
Serikali ya Qatar inajenga bandari mpya katika eneo la jangwa, mradi unaogharimu Dola za Marekani 80 bilioni na ikimteua raia wa Tanzania asimamie kazi hiyo.
Ujenzi huo unatokana na Serikali ya nchi hiyo kuamua kuhamisha bahari na kuipeleka katika eneo hilo la jangwa. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliyemaliza ziara ya
kuzitembelea nchi za Falme za Kiarabu juzi usiku, alitembelea mradi huo
wa bandari mpya ambao unajengwa eneo la jangwa na baadaye kuelekeza maji
ya bahari kufika eneo hilo.
Akizungumza na gazeti hili, Meneja wa mradi huo,
Potty Msuku alisema kazi kubwa anayofanya ni kusimamia na kuhakikisha
kazi inakwenda kwa wakati. Alisema bandari hiyo itakayoanza kufanya kazi kuanzia mwakani, ina magati zaidi ya 10 ya kuegeshea meli.
“Ninachoshukuru ni kwamba tuko mbele ya muda tuliopewa, tunakwenda vizuri.”
Mtanzania huyo alisema mpango wa ujenzi wa bandari
hiyo mpya ulibuniwa na Serikali ya Qatar ili kufungua lango la biashara
kwa mataifa makubwa. Alisema mradi huo ukikamilika utaifanya Qatar kuwa
moja ya mataifa yenye bandari kubwa dunia sanjari na mataifa ya
Kiarabu, Dubai na Abu Dhabi.
“Tumechimba eneo hili ambalo hadi Aprili mwakani tutakuwa tumepasua mwamba wa bahari na maji yatakuja huku,” alisema.
Alisema ujenzi huo ulioanza 2011 utakamilika 2016.
Alisema ujenzi huo ulioanza 2011 utakamilika 2016.
Msuku ambaye ni mhandisi kitaaluma, alisema ujenzi
wa bandari hiyo unakwenda kwa awamu, nyingine inayofuata ni ya
kuiunganisha bandari hiyo na reli na uwanja wa ndege utakaojengwa karibu
na eneo.
“Kazi kubwa inayoendelea sasa ni ya kuchimba kina,
tumefikia pazuri na nyingine ni kujenga eneo la biashara huru na
kitengo cha makontena.”
CHANZO: MWANANCHI
Msuku alisema sehemu kubwa ya wafanyakazi wanaojenga bandari
hiyo wengi wanatoka katika mataifa mbalimbali duniani ikilinganishwa na
raia wa nchi hiyo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati akipokea taarifa
za ujenzi huo, alielezea kuvutiwa na jinsi bahari itakavyohamishiwa
jangwani kwa ajili ya bandari hiyo. “Tumesikia nyumbani wanataka kujenga Bandari Bagamoyo, tutakuja, lazima tuendeleze nchi yetu,” alisema. Wakati huohuo, Waziri Mkuu, juzi usiku alihitimisha ziara yake hapa Qatar kwa kukutana na jumuiya ya wafanyabiashara.
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment