Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akizungumza na Kaimu Meneja wa
Mgodi wa Uchimbaji Kokoto wa Kongolo Uswisi mkoani Mbeya, Juma Michael
wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Miundombinu, juzi.
Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe
amesema hatosita kuwatimua kazi watendaji wabovu wa Shirika ya Reli
Tanzania na Zambia (Tazara) wanaoshindwa kusimamia kikamilifu utendaji
kazi wao na kuisababishia Serikali hasara ya mabilioni ya fedha kwa
masilahi binafsi.
Dk Mwakyembe aliyasema hayo wakati wa ziara yake
ya kikazi na Kamati ya Bunge ya Miundombinu walipotembelea Mradi wa
Mgodi wa kiwanda cha kuzalisha kokoto wa Kongolo uliopo katika Kijiji
cha Mswiwi sambamba na kukagua karakana ya Tazara.
Alisema utendaji kazi kwa mazoea ni changamoto
ambayo Serikali inapaswa kuisimamia na kuwawajibisha watendaji
wataobainika kuisababishia hasara kwa makusudi. Alisema Mkoa wa Mbeya ni miongoni mwa mikoa yenye
wawekezaji wengi wanaofanya biashara ndani na nje ya nchi na kwamba
wanalazimika kusafirisha mizigo yao kwa kutumia magari makubwa ya mizigo
huku wakikwepa kutumia reli kwa sababu ya ukubwa wa gharama za
usafirishaji.
Mjumbe wa kamati hiyo, Mbunge wa Viti Maalumu,
Rebecca Michael Mngodo alisema Serikali inaangalia uwezekano wa kutenga
fedha katika bajeti bungeni ili Tazara iweze kujiendesha yenyewe na
kuachana na mvutano uliopo baina ya Tanzania na Zambia hali inayosababisha uchumi wa nchi yetu kuporomoka.
“Jamani sisi wenyewe wabunge tumefika na
tumejionea hali halisi ya shirika letu ni hoi na kwamba huko tuendapo
tukatafakari nini kifanyike ili tuinusuru na tuangalia mfumo mwingine wa
kuiendesha kutokana na wenzetu wa zambia kukata mawasiliano ya
ushirikiano”alisema.
Naye Mbunge wa Ileje (CCM) na Mjumbe wa kamati ya
bunge Miundombinu ,Aliko Kibona aliomba Serikali kuangalia kwa jicho la
huruma swala zima ya upatikanaji wa mishahara ya wafanyakazi ,na huduma
za afya kwani hiyo na changamoto kubwa inayowakumba wafanyakazi wa
Tazara.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment