Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene.
Serikali iko mbioni kufuta mikataba ya
wakandarasi walioshindwa kukamilisha kazi ya kusambaza umeme vijijini
kwa wakati uliopangwa.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene
alisema hayo juzi alipohutubia wananchi wa Kata ya Mlunduzi wilayani
Mpwapwa Mkoa wa Dodoma baada ya kukagua miradi ya umeme.
Alisema katika maeneo mengi kazi hiyo imesimama huku wakandarasi wakilipwa fedha nyingi.
“Serikali haiko tayari kucheka na wakandarasi
wazembe wanaoshindwa kwenda na kasi inayotakiwa. Natangaza kuanzia leo
kuwa tutawafutia mikataba na watarudisha fedha ya umma,” alisema
Simbachawene.
Waziri alisema wakandarasi hao wamekuwa wakipoteza
muda kwa kuzunguka wakati wote, huku nguzo zikiwa zimelazwa chini na
wananchi ndiyo walinzi.
Mkazi wa Mlundizi, Jackson Lengwa alisema wamekuwa
wakishangazwa na Serikali kujisifu kuwa umeme unasambazwa wakati
wakandarasi hufanya kazi wanapowaona viongozi.
Lengwa alisema kauli ya Waziri Simachawene itakuwa na maana zaidi endapo itatekelezwa kwa vitendo.
Mwakilishi wa Kampuni ya Derm Electricity, Aziz
Msuya alisema usambazaji wa umeme wilayani Mpwapwa umefikia asilimia 52
ingawa kwa Mkoa wa Dodoma wamesambaza kwa asilimia 75. Msuya alisema wanafanya juhudi kubwa kuhakikisha
kazi hiyo inakwisha kwa wakati waliokubaliana na Serikali na
hawatakubali kukatisha mikataba yao.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment