Mahasimu wao katika kundi C Ghana na Afrika kusini hazijaamua nani 
atakuwamo katika vikosi vyao. Maandalizi ya fainali za kombe la mataifa ya Afrika yanaendelea, wakati 
timu inayopigiwa upatu kutoroka na kombe hilo Algeria imetaja kikosi 
chake cha mwisho kwa ajili ya fainali hizo mwakani nchini Guinea ya 
Ikweta 
Kocha mpya wa Ghana Avram Grant, ambaye 
aliiongoza Chelsea katika fainali ya kombe la Champions League mwaka 
2008 na kushindwa kwa penalti dhidi ya Manchester United , amechagua 
kikosi cha kwanza cha wachezaji 31.
Kocha wa Afrika kusini , Ephraim "Shakes" Mashaba , amewaita wachezaji 
34 kwa ajili ya kambi ya mazowezi baada ya krismasi mjini Johannesburg.
Cape Verde , Gabon na Mali tayari zimekwisha chagua vikosi vyao vya 
mwisho kwa mashindano hayo ya kila baada ya miaka miwili yanayojumuisha 
timu 16 zinazopambana katika fainali hizo katika viwanja vya mjini Bata,
 Ebebiyin, Malabo na Mongomo nchini Guniea ya Ikweta.
Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, mwenyeji Guinea ya Ikweta, Guinea na 
Cote D'Ivoire bado hazijataja vikosi vyao kabla ya muda wa mwisho wa 
Januari 7 wa kutangaza vikosi vyote vitakavyoshiriki katika fainali.
Kocha wa Algeria mzaliwa wa Ufaransa Christian Gourcuff amewajumisha 
wachezaji 18 kati ya kikosi cha wachezaji 23 waliokwenda Brazil mwaka 
2014 katika kombe la dunia na kuifikisha timu hiyo ya kaskazini mwa 
Afrika katika duru ya mtoano kwa mara ya kwanza.
Grant amewaondoa kundini Kevin-Prince Boateng na Sulley Muntari, ambao 
waliondolewa katika kikosi cha kombe la dunia nchini Brazil, baada ya 
kudokeza kuwa angependa kuwaita tena wachezaji hao.
Mchezaji wa siku nyingi wa kati Michael Essien , ambaye alicheza chini 
ya Grant akiwa Chelsea , ni mchezaji nyota mwingine ambaye ameshindwa 
kuingia katika kikosi hicho.
CHANZO: DW KISWAHILI
 
No comments:
Post a Comment