Social Icons

Pages

Thursday, December 18, 2014

WAARABU WATOA MASHARTI BANDARI YA BAGAMOYO

 
Maofisa wa eneo huria la uwekezaji la Jafza katika Bandari Jebel Ali ya jijini hapa wamelalamikia urasimu katika maeneo mbalimbali ya uwekezaji Tanzania na kudai kuwa ndiyo yanayokwamisha shughuli nyingi za maendeleo.

Maofisa hao wameitaka Serikali ya Tanzania kujenga Bandari ya Bagamoyo ili kuvutia wawekezaji badala ya kusubiri ijengwe na wawekezaji hao.
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya DP World wanaoisimamia Bandari ya Dubai, Mohamed Sharaf alisema hayo jana wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda na ujumbe wake walipotembelea bandarini hapo ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku saba ya kujenga uhusiano na kutafuta maeneo ya uwekezaji.
Sharaf alisema walifika Tanzania kutafuta maeneo na kufahamu utaratibu wa namna gani wanaweza kuwekeza, lakini walikatishwa tamaa na urasimu uliopo kutoka kwa baadhi ya watendaji.
Alisema kama Serikali ya Tanzania itafanikiwa kudhibiti hali hiyo, huenda wawekezaji wengi watajitokeza kuwekeza.
Akizungumzia ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ambayo Serikali imeingia ubia na China, aliishauri ikamilishe ujenzi kabla ya kuwakaribisha wawekezaji.
na imewezesha kuunganisha mataifa zaidi ya 130 duniani yanayoitumia bandari hiyo.
Sharaf alisema hadi sasa kitengo cha makontena kimeboreshwa na kinauwezo wa kuhudumia makontena milioni 15 kwa mwaka, hatua ambayo imerahisishwa na ufanyaji kazi kwa njia ya mtandao.
“Tunafanya kazi usiku na mchana, kwa sasa kuna kazi (transactions) zaidi ya milioni 18 ziko kwenye mtandao duniani, ndizo zinazofanya kazi ya kuliingizia fedha Taifa letu,” alisema.
Mapema jana asubuhi, Waziri Mkuu alikuwa na mazungumzo na Maofisa Watendaji Wakuu wa Emirates National Oil Company (ENOC), Said Foemy na Fandraj Govindaraj kabla ya kutembelea Kituo cha Biashara Dubai na kuonyeshwa mpango wa kituo hicho kujenga mji wa kisasa pamoja na uwanja wake wa ndege.\

CHANZO: MWANANCHI

No comments: