Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec)
Utangazaji wa matokea Jimbo la Mbagala ngazi ya
ubunge imeshindikana baada ya mawakala na wabunge wa jimbo hilo kutoa
mashariti matatu ikiwamo la kutaka uchaguzi huo kurudiwa.
Hatua hiyo imemfanya Mkurugenzi wa Uchaguzi Majimbo ya Temeke na Mbagala, Fotidus Kagimbo, kuahirisha kuendelea na mchakato wa kuhesabu kura za wabunge katika jimbo hilo na kuhaidi kutoa msimamo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) leo asubuhi.
Hatua hiyo imemfanya Mkurugenzi wa Uchaguzi Majimbo ya Temeke na Mbagala, Fotidus Kagimbo, kuahirisha kuendelea na mchakato wa kuhesabu kura za wabunge katika jimbo hilo na kuhaidi kutoa msimamo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) leo asubuhi.
Kagimbo alisema wakiwa katika chumba cha kuhesabia kura, mawakala
hao na wabunge waligomea kuendelea na kazi ya kuhesabu kura kwa madai
kuwa mchakato huo uligubikwa na dosari nyingi.
Alisema kutokana na hali hiyo, waliitaka Nec kurudia uchaguzi huo
ama kuendelea na kazi ya kuhakiki kwa kata zenye dosari, huku wengine
wakitaka kazi ya kuhakiki kura ianze upya kwa kata zote 10.
Kagimbo alisema suala la kurudia uchaguzi hawezi kulitolea majibu
ya hapo hapo hadi atakapowasiliana na uongozi wa juu, huku suala la
kuhakiki kata zote ni suala litakalochukua muda mrefu.
“Nec tumeshindwa kuendelea na kazi ya kumtangaza mshindi ngazi ya
ubunge katika Jimbo la Mbagala kutokana na mawakala na wabunge wa vyama
husika kutoa masharti au mapendekezo matatu ambayo siwezi kuyaamua mimi
hadi ngazi husika itamke. Hivyo naahirisha kazi hii hadi kesho asubuhi
(leo),” alisema Kagimbo.
Mgombea ubunge kwa Chama cha Wananchi (CUF), Kondo Bungo, alisema
dosari zilizojitokeza katika uchaguzi huo ni pamoja na kupotea kwa
makaratasi 24 yenye idadi ya wapigakura katika kata ya Mbagala Kuu.
Alisema dosari nyingine ni kuwapo kwa taarifa za uongo ikiwamo ya
yeye kupata kura moja katika kata ya Tuangoma huku nakala aliyokuwa nayo
ikionyesha amepata kura 78.
Alisema dosari nyingine ni pamoja na makaratasi yenye majumuisho ya
kura kutoka kata mbalimbali kutokuwa na saini za mawakala, jambo ambalo
hajawahi kupewa taarifa yoyote kutoka kwa wakala wake kuwa hawakusaini
karatasi hizo.
Kwa upande wake, mgombe ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Issa
Mangungu, alisema uchaguzi ulikuwa wa haki na ana imani kuwa ameshinda
hivyo wafuasi wa CUF wameanzisha malalamiko ili urudiwe.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment