Waandishi na wazungumzaji wengi hawako makini na
hawajali kuzingatia ufasaha wa Kiswahili. Nilieleza kidogo katika makala
zangu zilizopita kwamba watangazaji hasa wa redio na runinga
zilizosajiliwa katika miaka ya hivi karibuni ndio wasiotilia mkazo
matumizi fasaha ya Kiswahili.
Swali la kujiuliza ni kwa nini Watanzania wengi hasa wasomi hawathamini Kiswahili kama inavyostahili? Swali hili ni vigumu kulijibu lakini kwa kusoma makala haya labda utapata jibu.
Swali la kujiuliza ni kwa nini Watanzania wengi hasa wasomi hawathamini Kiswahili kama inavyostahili? Swali hili ni vigumu kulijibu lakini kwa kusoma makala haya labda utapata jibu.
Nimewahi kuandika kuwa kuchanganya Kiswahili na
Kiingereza katika kuandika habari makala au katika mzungumzo rasmi ni
kukidhalilisha Kiswahili. Waandishi na wazungumzaji wengi hawako makini
na hawajali kuzingatia ufasaha wa Kiswahili. Nilieleza kidogo katika
makala zangu zilizopita kwamba watangazaji hasa wa redio na runinga
zilizosajiliwa katika miaka ya hivi karibuni ndio wasiotilia mkazo
matumizi fasaha ya Kiswahili. Hii innatokana na vyuo vya uandishi wa
habari kutotilia mkazo mafunzo ya lugha kwa wafanyakazi wao ili kuwainua
kitaaluma zao. Viongozi wa vyombo vya habari wanatakiwa kuwaandalia
semina na warsha za kuboresha taaluma yao katika fani za uandishi na
utangazaji.
Nitatoa mifano michache ya makosa yanayofanywa na watangazaji wa runinga na redio. Kwa mfano utawasikia watangazaji wakisema:
- Message unazopeleka ni za nani ?
- I remember kwenye semina ya ndoa mambo yalikuwa safi.
- Lakini a good office is well arranged
- Hiyo intrastructure ni mbovu.
- Lazima ufokasi kwenye future na maelezo mengine mengi.
Mifano hii michache inaonyesha jinsi
tunavyoidhalilisha lugha yetu. Hivi kweli mzungumzaji alishindwa kupata
visawe vya maneno kama ‘message, remember, infrastructure, a good
office’ nk.? Kama ikishindikana angeweza kuwauliza wenzake wamsaidie
na pengine angeweza kutumia kamusi. Polepole anajiongezeaauwezo wa
kitaaluma ambao ni hazina kubwa kwake. Mazoea ya kujielimisha ama kwa
kusoma au kuwatumia wenye ujuzi zaidi ni njia mojawapo ya kujijenga kwa
kuongeza maarifa.
Pamoja na hayo liko kundi jingine ambalo lina
sauti kubwa katika jamii. Kundi hili ni la wanasiasa na hasa wabunge
ambao wanaokuwa wakijadili hoja zao wanapokuwa bungeni au
wanapowahutubia wananchi. Wanasiasa hawa nao wanavunja maadili ya lugha
kwa kuchanganya Kiingereza na Kiswahili katika mazungumzo yao. Watambue
kuwa wanasikika kwa jamii nzima ya Watanzania na pia nje ya nchi kwani
watu huwa macho kufuatilia kinachozungumzwa bungeni au kwenye mikutano.
Baadhi ya wanasiasa wanapozungumza hawako makini katika kuchagua
misamiati au istilahi za kutumia. Kwa kuwa muda wa kuzungumza ni mfupi,
wanachokabiliana na tatizo la uhaba wa maneno na hivyo uchaguzi wa
maneno wanayotumia unawatatiza. Inashangaza kuona kuwa ile kanuni kwa
wabunge kuwa wawapo bungeni wana uhuru wa kutumia Kiswahili au
Kiingereza. Kwa hiyo matumizi ya lugha hizi mbili kwa ufasaha
umekubalika bungeni. Hivyo uteuzi wa lugha moja ni wa hiyari ila
kuchanganya lugha hizi mbili katika kufafanua jambo ni makosa.
Ninavyofahamu ni kuwa kama mbunge akiamua kutumia Kiswahili basi
aendelee kukitumia moja kwa moja. Kama anataka kutumia Kiingereza basi
atumie Kiingereza moja kwa moja. Ila kuchanganya lugha hizi mbili kwa
pwakati mmoja katika majadiliano ni kuwakosea haki baadhi ya
wasikilizaji.
Swali la kujiuliza ni kwa nini wanasiasa,
wanataaluma na watangazaji siku hizi hawana umakini katika matumizi ya
lugha fasaha na sanifu wanapoelezea jambo kwa Watanzania na dunia kwa
jumla? Ijapokuwa sijafanya utafiti wa kina lakini kwa uzoefu wangu wa
miaka mingi katika fani hii ya matumizi ya Kiswahili katika shule na
vyuo, nimegundua kuwa vijana wengi wanataka kujifanya kuwa wao ni
wasomi hata kama wamefikia kidato cha nne au sita. Ukweli ni kuwa kama
una elimu ya sekondari na hata ya chuo kikuu bado huna haki ya kujigamba
kuwa wewe ni msomi. Inashauriwa kuwa kujielimisha ni wajibu wetu sote
kwani hatuko wakamilifu. Sifa mojawapo ya kuwa msomi ni kuzungumza lugha
rahisi na inayoeleweka kwa jamii nzima ya wasikilizaji wako.
Nimewasema watangazaji katika vyombo vyetu vya
habari pamoja na wanasiasa lakini ingekuwa bora zaidi na kwa ajili ya
manufaa ya umma kama serikali ingekuwa na sera ya lugha inayotakiwa
kufuatiliwa kwa makini. Nafahamu kuwa serikali imeunda Baraza la
Kiswahili la Taifa kama chombo cha kusimamia na kuratibu Kiswahili
Tanzania tangu mwaka 1967 lakini hakina meno. Ili sheria ya kuliunda
Baraza la Kiswahili la Taifa liwe na meno, inatakiwa ifanyiwe
marekebisho ya kuliwezesha kuchukua hatua za kisheria endapo asasi,
taasisi, idara, kampuni au mtu binafsi atafanya makosa ambayo
itajulikana ni ya kizembe, achukuliwe hatua. Hii ina maana kuwa na
sheria iwafanye viongozi, waandishi na watangazaji kuwajibishwa kama
vile kupewa maonyo, kufungiwa kwa muda au kufutiwa liseni zao moja kwa
moja endapo watakiuka kanuni zilizowekwa.
Nimewasema wanasiasa, waandishi na watangazaji
pamoja na serikali kila moja kutimiza wajibu wake. Hata hivyo, ieleweke
kuwa hayupo mtu au chombo cha kunyooshewa kidole. Wote tuna wajibu wa
kuona kuwa tunaithamini lugha yetu na huo ndiyo uzalendo tunaoupigania.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment