Kutoka kushoto ni Rais wa Uganda ,Yoweri Museveni, Rais Jakaya
Kikwete na Rais wa Burundi Pierre Nkurunzinza walipokutana jijini Dar es
Salaam kuhimiza uimarihshaji wa miundombinu ya barabara na reli ili
kuimarisha uchumi wa nchi hizo.
Mkutano wa marais wa nchi zinazounda Ukanda wa
Kati wa Kibiashara, Barani Afrika, wamekutana jijini Dar es Salaam na
kuweka mikakati mbalimbali ya kukuza sekta ya miundombinu ya barabara na
reli, kwa manufaa ya mataifa hayo.
Mkutano huo wa siku mbili umehudhuriwa na Rais
Jakaya Kikwete, Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, Rais wa Burundi, Pierre
Nkurunziza, Rais wa Rwanda, Paul Kagame na Waziri wa Uchukuzi wa
Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo (DRC), Justine Kanumba kwa niaba Rais
Joseph Kabila.
Uzinduzi wa reli
Rais Kikwete na Rais Nkurunziza wamefungua ukurasa
mpya wa kuzindua safari za moja kwa moja za treni za mizigo kutoka Dar
es Salaam kwenda nchi za Burundi na Uganda. Nyuso za furaha zinatawala wakati wa uzinduzi huo.
Katika kulionyesha hilo, marais hao wanainua bendera za rangi ya kijani
juu kuonyesha kuruhusu treni hiyo yenye uwezo wa kubeba makontena kati
ya 10 na 15.
“Awali safari za treni za mizigo zilikuwa
zikichukua wiki mbili kufikisha mizigo kwenye nchi husika, lakini kwa
sasa zitakuwa zinachukua siku mbili pekee,” anasema Rais Kikwete.
Rais Nkurunziza anasema kuanza kwa safari hizo za
kuelekea nchini kwake ni jambo la kujivunia kwa kuwa awali mizigo
ilikuwa ikichukua muda mrefu, lakini uamuzi wa Serikali ya Tanzania
kupunguza muda wa safari hizo kutoka wiki mbili hadi siku mbili una
faida kwa pande zote mbili. “Safari hizo zitasaidia nchi yangu kusafirisha mizigo mingi na kwa njia ya kwa haraka,” anasema Rais Nkurunziza.
Rais Kikwete anasema Serikali yake imenunua injini
13 za treni na kwamba, kati ya hizo mbili ziliwasili nchini wiki mbili
zilizopita. Zingine tano, anasema zinatarajia kuwasili nchini mwezi huu
na zilizobaki zitaletwa mwezi ujao. Zaidi ya hayo anasema wamenunua mabehewa 274 na kati yake, 150 yaliwasili nchini Februari mwaka huu. Rais Kikwete anasema anatamani ifike siku moja,
Tanzania iwe na treni ya mizigo ya ghorofa tatu, yenye mabehewa mia,
inayoweza kuchukua makontena mia tatu, ili kurahisisha usambazaji wa
mizigo toka Bandari ya Dar es Salaam kwenda mikoani na nchi jirani.
Hata hivyo, anasema ili kutekeleza mipango hiyo
yenye manufaa kwa nchi za ukanda wa kati kwa ufanisi, ni vyema kuwa na
wazo la Serikali kuwa mmiliki wa reli, lakini biashara isimamiwe na
sekta binafsi.
Kuondoa vikwazo
Reli ya kisasa
Bandari
Kuondoa vikwazo
Katika ufunguzi, Rais Kikwete anaainisha mikakati
mbalimbali iliyowekwa na Tanzania kuhakikisha miradi ya ukanda wa kati
iliyopo nchini inafanikiwa kwa faida ya nchi zote wanachama. Rais Kikwete anasema Serikali yake inakusudia
kuondoa kila kikwazo kilichokuwa kinakwamisha usafirishaji wa mizigo
kutoka bandari ya Dar es Salaam kwenda nchi jirani.
Anasema pia, Serikali imeamua kupunguza vizuizi
vya polisi barabarani kutoka 15 hadi vitatu na vituo vya mizani kutoka
10 hadi vitatu vitakavyojengwa vigwaza mkoani Pwani, Manyoni (Singida)
na Nyakahura (Kagera). “Kuna wakati tulikuwa na vizuizi 47 kila sehemu
unatoa kitu kidogo, lakini sasa tumeamua viwe vitatu. Pia, tutaanza
kutumia mizani ya barabarani ya kisasa,” anasema Rais Kikwete.
Reli ya kisasa
Ukanda wa kati unatarajia kutekeleza miradi 23
kwenye sekta ya uchukuzi. Kati ya hiyo, kilomita 2,707 za reli, kilomita
2,406 za barabara na bandari kubwa tatu zilizopo nchini.
Waziri wa Uchukuzi Samuel Sitta anasema ujenzi wa reli hiyo utaanza mwaka huu. “Tunatarajia kuanza ujenzi huo ndani ya mwaka huu.
Ifikapo Juni Rais Jakaya Kikwete atakwenda kuweka jiwe la msingi katika
kituo cha stesheni kule Mpiji ambako reli itaanzia,” anasema Sitta,
akifafanua kuwa mradi huo utagharimu Sh14 trilioni. Anasema ujenzi huo unatarajia kukamilika ndani ya
miaka mitano na utasaidia kukidhi mahitaji makubwa ya ubebaji wa mizigo
kwenda nchi za jirani kama Burundi, Rwanda, Uganda na Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo.
“Reli hiyo yenye uwezo wa kubeba treni yenye
mabehewa umbali kilomita moja kwa safari moja itasaidia pia katika
usafirishaji wa wananchi,” anasema Sitta. Anasema ujenzi huo ni mradi mkubwa zaidi kuwahi kuwekezwa nchini na utatekelezwa na kampuni mbalimbali za China.
Sitta anasema hadi sasa, Kampuni ya Rasilimali za Reli (Rahco)
imekamilisha taratibu za kumpata mshauri wa mradi huo ambaye ni Kampuni
ya Rothschild ya Marekani ambayo itawezesha kupata fedha za ujenzi wa
reli hiyo. Rais Kagame anapongeza mpango huo, akisema, ili
kuendana na kasi ya ukuaji wa uchumi, ni muhimu kuhakikisha miundombinu
ya uchukuzi hasa reli inaboreshwa.
Anasema maboresho na mikakati ya miundombinu hasa
wa kujenga reli ya kisasa ni hatua nzuri lakini jukumu hilo lisiachiwe
nchi moja pekee bali wahusika wote washiriki kikamilifu.
“Mkakati huu unahitaji ushirikiano kati ya
Serikali za nchi washirika pamoja na sekta binafsi kwa sababu inahitaji
uwekezaji mkubwa,” anasema Rais Kagame mbele ya wawekezaji zaidi ya 300
wa miradi 23 ya ukanda wa kati.
Rais huyo anasema umefika wakati kwa nchi wanachama kuhakikisha kuwa mipango yote inatekelezwa kwa wakati. “Siyo mara ya kwanza tunakutana kujadili masuala kama haya. Lakini sasa umefika wakati wa sisi kwenda mbele na siyo kurudi nyuma tena. Ukanda huu ni muhimu sana kwani unawaunganisha watu wetu pamoja, unasaidia kuchochea na kuongeza fursa mbalimbali za uchumi kwa nchi zetu,” anasema.
Rais huyo anasema umefika wakati kwa nchi wanachama kuhakikisha kuwa mipango yote inatekelezwa kwa wakati. “Siyo mara ya kwanza tunakutana kujadili masuala kama haya. Lakini sasa umefika wakati wa sisi kwenda mbele na siyo kurudi nyuma tena. Ukanda huu ni muhimu sana kwani unawaunganisha watu wetu pamoja, unasaidia kuchochea na kuongeza fursa mbalimbali za uchumi kwa nchi zetu,” anasema.
Anasema nchi wanachama wa ukanda wa huu wanapaswa
kutambua mchango wa uwekezaji katika ukanda huo kwani matunda yake
yataliwa kwa ujumla. Rais Museveni anasema hakuna namna ujenzi wa reli
unaweza kuepukika kwa kuwa barabara zinaharibika mara kwa mara huku
zikigharimu fedha nyingi.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Amina Mohamed
anasema miradi iliyoanzishwa chini ya jumuiya, itachangia sehemu kubwa
kuimarisha hali ya kiuchumi iliyokuwa imekwama kutokana na miradi ya
miundombinu kushindikana.
Bandari
Kuhusu ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam, Rais
Kikwete anasema idadi ya mizigo inayosafirishwa imeongezeka kutoka tani
milioni 9.2 mwaka 2010 hadi milioni 14, mwaka jana na kufikia mwishoni
mwa mwaka huu inatarajiwa kufikisha milioni 18.
“Idadi ya siku za kutoa mzigo bandarini zimepungua
kutoka siku 21 hadi 9 na bado tunataka zipungue zaidi. Kuhusu wizi
hakuna taarifa ya tukio lolote kwa miaka miwili sasa…Pia Serikali ina
mpango wa kujenga bandari mpya Bagamoyo itakayoweza kuhifadhi tani
milioni 240 kwa mwaka,” anasema Rais Kikwete.
Usalama bandarini
Kuhusu ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam, marais Kikwete na
Rais Kagame wanasema ufanisi uliopo bandarini hapo hivi sasa unaridhisha
na kwamba unaongeza kasi ya kukua kwa maendeleo ya nchi zote mbili.
Usalama bandarini
Rais Kikwete anazihakikishia nchi za Afrika
Mashariki na Kati kuwa kuna usalama wa uhakika wa mizigo yao katika
bandari ya Dar es Salaam.
Wakiwa katika kitengo cha kushusha na kupakia mizigo cha TICTS bandarini hapo, Rais Kikwete anasema uongozi wa bandari uliamua kuwatimua wafanyakazi ambao hawakuwa waaminifu. “Kwa hiyo kusikia habari nzuri zinazofanywa hapa mnanifurahisha sana. Kulikuwa na genge la wezi, sifa mbaya, meli zinakaa siku 23, mambo ya ajabu sana, leo meli zinakaa kwa muda mfupi na hakuna udokozi, kumbe mnaweza kuwa waaminifu,” anasema Rais Kikwete.
Wakiwa katika kitengo cha kushusha na kupakia mizigo cha TICTS bandarini hapo, Rais Kikwete anasema uongozi wa bandari uliamua kuwatimua wafanyakazi ambao hawakuwa waaminifu. “Kwa hiyo kusikia habari nzuri zinazofanywa hapa mnanifurahisha sana. Kulikuwa na genge la wezi, sifa mbaya, meli zinakaa siku 23, mambo ya ajabu sana, leo meli zinakaa kwa muda mfupi na hakuna udokozi, kumbe mnaweza kuwa waaminifu,” anasema Rais Kikwete.
Kwa upande wake, Rais Kagame anasema amefurahishwa na mafanikio yaliyofikiwa bandarini hapo kwa kuwa ni faida kwa Rwanda pia. “Napenda nimpongeze Rais Kikwete kwa mafanikio
yaliyopatikana bandarini, kazi ikiwa nzuri (bandarini Dar), huko kwetu
Rwanda tunafaidika,” anasema Rais Kagame.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPA, Awadhi Massawe
anasema ipo tofauti kubwa ya utendaji kazi kati ya Bandari ya Dar es
Salaam na Bandari ‘pinzani’ ya Mombasa nchini Kenya.
Anasema ingawa nchi za Maziwa makuu zinatumia
bandari hizo mbili, Bandari ya Dar es Salaam ndiyo inayosafirisha mizigo
mingi zaidi. Massawe anasema tangu kufanyika kwa maboresho
bandarini hapo, idadi ya mizigo inayopelekwa katika nchi za Rwanda,
Burundi, Kenya na Uganda, imeongezeka.
Mkurugenzi Mtendaji wa TICTS, Walles Paul anaiomba
Serikali kuongeza eneo la kufanyia kazi kwa maelezo kuwa uamuzi huo
utasaidia kuendeleza mafanikio yanayopatikana hivi sasa. “Nafasi haitoshi tunahitaji kuongezewa ili tusirudi nyuma tulikotoka,” anasema Paul.
Vikwazo vya kibiashara
CHANZO: MWANANCHI
Kwa upande wake, Rais wa Uganda, Yoweri Museveni
anatumia mkutano huo kuwakumbusha wanachama wa nchi za ukanda wa kati
kuvitazama kwa makini vikwazo vya kibiashara vinavyoweza kuwakwamisha.
Kiongozi huyo anataja vikwazo hivyo kuwa ni
ukosefu wa usalama katika nchi, wafanyakazi kukosa ujuzi unaostahili,
ukosefu wa masoko na kutopatikana kwa faida iliyokusudiwa.
Anasema ili mipango ya kibiashara inayopangwa na nchi hizo ifanikiwe lazima vikwazo vijulikane na kutafutiwa ufumbuzi mapema. “Wataalamu wa uchumi wanasema gharama ya usafiri
katika biashara inapaswa kuwa asilimia 40, mtaji asilimia 20, kazi
asilimia 10, ukilitimba asilimia tano, lazima tujiulize kikwazo kipi
kinatukwaza,” anasema Museveni.
Ukanda wa kati wa kibiashara ulianzishwa mwaka
2006 chini ya mapatano ya nchi tano za Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo, Rwanda, Tanzania na Uganda.
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment