
Mwenyekiti wa ACT, Anna Mghwira.
Chama cha ACT -Wazalendo, kimewataka Watanzania
kuipigia kura ya hapana Katiba Inayopendekezwa kwa sababu imeleta
mgawanyiko katika taifa kutokana na kupatikana kwa njia zisizo za
kiuadilifu na mchakato wake kuendeshwa kibabe.
Kadhalika, kimesema katiba hiyo haijajibu matakwa na malalamiko ya
wananchi kwenye masuala ya mbalimbali, ikiwamo muundo wa serikali, miiko
na maadili ya viongozi wa umma, haki za binadamu, madaraka ya Rais na
uwiano wa muhimili wa dola.
Mwenyekiti wa ACT, Anna Mghwira, alisema jana kwa waandishi wa habari, kuwa: “Suala la Katiba, tumeamua kuwa tutaanza nalo mara ya kukamata
dola, tutaanzia pale alipoishia Jaji Joseph Warioba, hii inatokana na
ukweli kwamba mchakato wa uundaji wa Katiba mpya ulifanywa batili na
hatua zilizofuatwa baada ya rasimu ya pili kukamilika.”
Anna, alisema azimio lingine la mkutano wa Kamati Kuu ni kumuagiza
Katibu Mkuu wake, Samson Mwigamba, kutangaza nafasi ya kuwapata wajumbe
watakaoingia kwenye kamati ya uadilifu ya chama taifa, mchakato ambao
utaanzia ngazi za chini za chama.
Pia, kamati hiyo iliazimia kuanza ziara katika mikoa 10 mara baada
ya kumalizika kwa sikukuu ya Pasaka, lengo likiwa ni kukitangaza chama,
kutambulisha viongozi na kutangaza Azimio la Arusha lililohuishwa baada
ya kupitishwa na vikao vya chama na kwamba kwa sasa linachapwa.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment