Rais Barack Obama leo anakutana na viongozi wa baraza la Congress,
lakini anakabiliana na hadhara tofauti kabisa, licha ya kuwa orodha ya
wageni wake hao haijabadilika.
Mkutano wa rais Obama na viongozi wa baraza la wawakilishji na seneti ni
wa kwanza tangu pale baraza la Congress linalodhibitiwa na chama cha
Republican kufanya kikao chake cha kwanza wiki iliyopita. Kiongozi wa maseneta wa chama cha Democratic Harry Reid , mshirika wa
siku nyingi wa rais Obama katika baraza la seneti, alishushwa cheo
katika uchaguzi wa Novemba mwaka jana na kuwa kiongozi wa wachache
katika seneti. Kiongozi wa upinzani Mitch McConnel , ambaye ni mwiba
katika upande wa Obama kama kiongozi wa wachache katika baraza la seneti
, sasa amechukua wadhifa wa zamani wa Reid katika baraza hilo la juu.
Mazungumzo ya fursa za ushirikiano
Watu hao watatu watajiunga na spika wa bunge John Boehmer na kiongozi wa
wabunge wa chama cha Democratic Nancy Pelosi katika ofisi ya rais
kujadili fursa za uwezekano wa ushirikiano kati ya chama cha Democratic
na Republican mwaka huu. Hata hivyo haifahamiki bado kwamba vyama hivyo viwili vitaweza kufumbia
macho tofauti zao za wazi katika masuala kadhaa na kuangalia katika
maeneo machache ya msimamo wa pamoja. Vyama vyote viwili vilimaliza uchaguzi wa muhula wa kati mwaka jana
vikizungumzia kwa matarajio juu ya kufanyakazi kwa pamoja kuhusiana na
mageuzi ya kodi, kukuza biashara na maendeleo ya miundo mbinu - maeneo
ambayo Obama na Warepublican wanaweza kwa kiasi fulani kukubaliana. Lakini mwanzoni mwa mwaka huu umetamalaki kwa kiasi kikubwa na mapambano
yale ambayo yanatambuliwa kuhusiana na bomba la Keystone XL, hatua za
Obama kuhusu wahamiaji pamoja na sera zake za mambo ya kigeni.
Nafasi ya maafikiano
Katika muda wa wiki mbili zilizopita, Obama mara kwa mara ametishia
kuchukua hatua ya kutumia kura yake ya turufu kuzuwia miswada ambayo
Warepublican wameiwasilisha kama masuala yao ya umbele. Hata hivyo , msemaji wa Ikulu ya Marekani Josh Earnest amesema kuna "
mambo chungu nzima" ambayo Obama anaweza kuyafanya mwaka huu pamoja na
Warepublican. "Haina maana tutakubaliana na kila kitu - kwa hakika hilo haliwezekani,"
amesema Earnest. " Lakini suala ni kwamba , tutaruhusu hali ya
kutokubaliana kuhusu masuala machache na kuwa chachu cha kufikiwa
makubaliano mengine yote. "Rais anahakika kwamba hilo halitatokea," ameongeza. Haijafahamika wazi iwapo Reid atahudhuria kikao hicho. Anapata nafuu
kutokana na maumivu yanayohusiana na mazowezi na msemaji wake amekataa
kusema iwapo atakuwapo katika mkutano huo.
CHANZO: DW KISWAHILI
No comments:
Post a Comment