Polisi
 mjini Manila wamevamia gereza moja na kuushangaza umma wa Philippines 
baada ya kung'amua maisha ya anasa yanayoendelea ndani ya gereza hilo 
kwa kikundi cha baadhi ywa wafungwa wenye upendeleo wa kipekee.
Uvamizi
 huo umefanywa katika gereza hilo la Bilibid lenye wafungwa wengi nchini
 humo kufuatia taarifa kwamba mtandao wa dawa za kulevya nchini humo 
unafanya kazi katika gereza hilo kwa njia za panya.
Baada ya 
uvamizi huo maafisa wa polisi walikuta wafungwa hao wakiwa wamefunga 
viyoyozi,mabafu ya kuogea ya kisasa yenye marumaru na kupambwa kwa mawe 
ya thamani,makasha ya kuhifadhia fedha,saa za gharama na fedha lukuki.
Wafungwa
 hao walifanikiwa pia kununua pombe kali za gharama kubwa ,komputa na 
hata simu za kisasa za gharama kubwa.kufuatia tukio hilo serikali ya 
Philippine imeahidi kufanya uchunguzi wa kina.
CHANZO: BBC SWAHILI 
No comments:
Post a Comment