Yanga imefanya usajili wa
kushtukiza kwa kumsajili Amissi Tambwe aliyeachwa na Simba huku kibarua
cha Mbrazili Marcio Maximo kikiwa dakika za mwisho Jangwani.
Habari za ndani kutoka Yanga zinasema kuwa Tambwe alisaini mkataba wa mwaka mmoja jijini Dar es Salaam jana. Kutokana na kusajiliwa kwa Tambwe, Yanga imemkata
Mbrazili mwingine, Emerson Roque, ambaye alikuwa akibebwa na Maximo
licha ya uongozi kutomfurahia. Tambwe, ambaye alifunga mabao 19 msimu uliopita
akiwa na Simba alitemwa na Simba na nafasi yake kuchukuliwa na Simon
Sserunkuma aliyeng’ara katika mchezo wa Nani Mtani Jembe, Jumamosi. Asaini Yanga, Maximo nje katika hatua nyingine,
kocha wa Yanga, Marcio Maximo amegomea mpango wa uongozi wa klabu hiyo
wa kutaka kumrejesha aliyekuwa kocha msaidizi Charles Boniface Mkwasa
katika benchi la ufundi.
Uongozi wa Yanga kwa muda mrefu unataka kumpa
jukumu Mkwasa la kumsaidia Maximo ili kuimarisha benchi hilo kutokana na
ukweli kuwa enzi ya Mkwasa na aliyekuwa mkuu wake, Hans Van Pluijm,
klabu hiyo ilikuwa moto wa kuotea mbali pamoja na kushindwa kutwaa
ubingwa.
Uamuzi huo umetokana na mwenendo wa klabu hiyo kwa
sasa ambapo pamoja na kushika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu
Tanzania Bara, imani ya mashabiki na wanachama ya kufanya vizuri msimu
huu imetoweka kutokana na timu inavyocheza iwe katika mechi za kirafiki
na za kimashindano.
Habari za uhakika kutoka klabuni hapo zimesema
kuwa Maximo ametoa sharti la kuvunja mkataba wake na klabu hiyo endapo
uongozi utamrejesha Mkwasa katika timu hiyo kwani yeye tayari ana mfumo
wake na kocha wa sasa, Leonaldo Neiva.
Mmoja wa viongozi wa Yanga alisema kuwa Maximo
ameshtukia ‘janja’ hiyo kwani anajua fika baada ya Mkwasa, itafuata zamu
ya Pluijm kuingia katika timu hiyo na yeye ’kurushiwa’ virago vyake.
“Juzi (Jumapili) kulikuwa na tetesi hizo na baadhi ya viongozi wa Yanga
kukutana na kocha kujadili masuala hayo lakini kikao hakikumalizika kwa
maridhiano na hii imetokana na msimamo wa Maximo ambaye amesimama katika
falsafa yake,” alisema. Akizungumzia taarifa hizo, Mkwasa alisema kuwa hajui lolote
kuhusiana na yeye kujiunga na Yanga na kama ipo nafasi hiyo, basi yeye
hajaambiwa.
CHANZO: MWANANCHI
“Sijui lolote, ila kwa methali zetu, lisemwalo
lipo na kama halipo linakuja, ila kiukweli kabisa, sijui lolote na hata
huyo Hans Van Pluijm ambaye anatajwa kuwa yupo hapa nchini, hayupo, kama
angekuwepo, lazima angewasiliana na mimi,” alisema Mkwasa. Kwa upande wake, Maximo hakuwa tayari kuzungumzia
suala hilo na kusema anaheshimu utaratibu wa klabu. “Kuna taratibu za
klabu, nafasi yangu ya kuzungumza ni baada ya mechi au kwenye mkutano na
waandishi wa habari, naheshimu utaratibu huo,” alisema Maximo.
Naye kocha wa Simba, Patrick Phiri ameshangazwa na
kitendo cha Yanga kutaka kumfungashia virago Maximo kwa kusema klabu
hiyo inafanya uamuzi wa haraka. Phiri alisema kumfukuza Maximo si sababu ya Yanga
kupata ushindi na kusisitiza kuwa kufungwa mechi ya Mtani Jembe pia si
kipimo cha kumwona Maximo hafai na kupuuza mchango wake. “Huo ni uamuzi wa haraka wanaotaka kufanya Yanga.
Maximo ni kocha mzuri na mwenye kiwango kikubwa, viongozi wanapaswa
kutambua mechi ya Simba na Yanga ni kubwa, leo Simba imeshinda kesho
Yanga itashinda, Simba kumfunga Yanga au Yanga kumfunga Simba ni matokeo
ya mpira.”
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment