Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari
ilieleze kuwa, Profesa Assad kwa sasa yupo nchini Uingereza kuhudhuria
mkutano wa vikao vya bodi hiyo ambayo wajumbe wake ni wadhibiti na
wakaguzi wakuu wa hesabu za Serikali kutoka Uingereza, Tanzania na
India.
Profesa Assad alisema ameridhishwa na mwenendo wa
vikao vya UNBoA na kuahidi kushirikiana kwa karibu kufanya kazi na
wajumbe wenzake wanaounda bodi hiyo.
“Nimeridhishwa na mwenendo wa bodi nawaahidi kufanya nao kazi kwa karibu na wajumbe wenzangu wote,” alisema Profesa Assad.
Nafasi ya uenyekiti wa UNBoA ilikuwa inashikiliwa
na CAG Amyas Morse wa Uingereza ambaye kwa pamoja na CAG Shashi Sharma
wa India wameahidi kumpa ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza
majukumu waliyomkabidhiwa.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment