
Miradi hiyo inatekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar
es Salaam (DAWASA) kwa msaada wa Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa
(UN-HABITAT) huku mradi wa uzalishaji wa umeme wa gesi asilia ya
kinyesi cha binadamu ukiendeshwa na Taasisi ya Kuendeleza Nishati Asilia
na Uhifadhi wa Mazingira Tanzania (Tatedo) katika shule hiyo.
Meneja mipango wa UN-HABITAT nchini, Phillemon Mutashubirwa,
alisema miradi hiyo ilienda sambamba na uchimbaji wa visima, ujenzi wa
minara ya kuwekea matenki ya kuhifadhi maji.
Mratibu wa Tatedo, Shima Sago, alisema wamegundua kuwa ni nishati
ya gharama rahisi ambayo ni ya kinyesi cha binadamu kutoka kwa wanafunzi
itakayokuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 200 za umeme na kuwa msaada
kwa shule hiyo.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment