Pages

Friday, April 10, 2015

HATUTAOGOPA CHANGAMOTO ZA TEKNOLOJIA: NCHEMBA

 
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, amesema serikali haitakimbia wala kuogopa ukuaji wa teknolojia nchini, bali inajipanga kupambana na changamoto zinazojitokeza katika teknolojia hiyo kwa kuwa inachangia katika ukuaji wa uchumi.Nchemba alisema hayo wakati akizindua huduma ya kifedha kwa njia ya mtandao ambayo imeshirikisha Benki ya NMB na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, itakayowawezesha wateja wake kutuma au kutoa fedha kutoka kwenye akaunti ya NMB kwenda kwenye akaunti zao za Airtel money kupitia simu za mkononi.
Alisema hakuna haja ya kupingana na ukuaji wa teknolojia isipokuwa kinachotakiwa ni kujiandaa kwenda sambamba na ukuaji huo kwa kujipanga ya kupambana na baadhi ya changamoto zinazojitokeza kwa kuwa inachangia kwa kiwango kikubwa ukuaji wa uchumi nchini.
Akitolea mfano suala la huduma za kifedha, Nchemba alisema mpaka sasa umesaidia wananchi wa mijini na vijijini kupata huduma hiyo kwa urahisi zaidi tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment