Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini
(Tanroads), Patrick Mfugale
Kituo kipya cha mzani cha Vigwaza
kilichopo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani, kitakachoanza kutumika hivi
karibuni kinatarajiwa kuwa mwarobaini wa uharibufu wa barabara
unaotokana na madereva hasa wa malori kuzidisha mizigo na kupelekea
baadhi ya barabara kuharibikia.
Pia kituo hicho, kilichotumia Sh11 bilioni kwenye
ujenzi wake kitasaidia kupunguza msongamano wa magari katika mzani
wakati wa kupima mizigo tofauti na ilivyo sasa. Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Patrick Mfugale aliwaambia waandishi wa habara jana kuwa,
mzani wa Vigwaza ni wa kisasa na wa kipekee nchini.
“Unaweza kupima gari moja kwa sekunde 30 badala ya dakika moja na nusu kama ilivyo kwa kituo cha zamani cha Kibaha.” Alisema, wanatarajia kwamba kituo hicho kitaonyesha ufanisi mkubwa na kuondoa matatizo yaliyopoa sasa.
“Unaweza kupima gari moja kwa sekunde 30 badala ya dakika moja na nusu kama ilivyo kwa kituo cha zamani cha Kibaha.” Alisema, wanatarajia kwamba kituo hicho kitaonyesha ufanisi mkubwa na kuondoa matatizo yaliyopoa sasa.
Kutokana na hilo, alisema kabla ya kuzinduliwa rasmi mzani huo wataanza na majaribio ya muda. “Hivyo magari yote yatapimwa pale. Kituo cha
Kibaha hakitatumika kwa muda hadi pale muda wa majaribio
utakapokamilika,” alisema na kuongeza kuwa uzinduzi utafuata baada ya
majaribio hayo.
Alifafanua kuwa, utaratibu za upimaji kwenye kituo
hicho utakuwa wa tofauti na kwamba magari yasiyozidisha uzito
yataendelea na safari na yaliyozidisha uzito yataelekezwa kwenye mzani
mkubwa kwa taa nyekundu ili yapimwe.
Pia kwenye mzani huo kutakuwa na kamera za CCTV kwa ajili ya kuhakikisha hakuna ukiukwaji wa sheria. “Dereva atakayeonyesha anataka kukwepa taa
nyekundu atalazimika kulipa tozo ya dola 2,000 za Kimarekani sawa na
Sh3.6 milioni,” alisema.
Mfugale alisema, magari yanayotakiwa kupimwa
kwenye mzani huo kwa mujibu wa sheria ya barabarani ni yale yote yenye
uzito unaoanzia tani tatu hadi tatu na nusu. Pia, alitumia nafasi hiyo kuwataka madereva
wanaoendesha magari hayo kuhakikisha wanaendesha magari kwenye upande
unaostahili bila kukanyaga mstari mweupe, kuzingatia mwendo wa kilomita
50 kwa saa. “Madereva wahakikishe matairi yanapia juu ya ‘plates’ za mashine ya kupima uzito, magari yao yaachane kwa umbali wa mita 30.
Iwapo gari likizuia magari mengine kwenye barabara
ya kuingilia kwenye mzani na hivyo kuzuia magari mengine dereva mwenye
gari hilo atatakiwa kulipa faini ya Sh300,000 au kifungo kisichopungua
mwaka mmoja,”alisisitiza Mfugale.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment