Social Icons

Pages

Monday, March 16, 2015

TIMU YA KUDHIBITI UJANGILI YABAINI SIRI YA MITANDAO

 
Rais Jakaya Kikwete.
Kikosi cha kupambana na ujangili nchini, kimebaini  mtandao wa majangili na kwamba kinafuatilia nyendo za mtuhumiwa na anayedaiwa kuwa kinara wa ujangili nchini (jina linahifadhiwa), mkazi wa Arusha.
Mkuu wa Idara ya Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) na Mratibu wa kikosi hicho, Robert Mande, aliwaeleza waandishi wa habari wa Chama cha Habari za Utalii nchini (TJT) kuwa mtandao huo umejigawa katika makundi matano tofauti.
Pia alisema kundi la sita la ujangili liko nje ya nchi.  Rais Jakaya Kikwete aliwahi alimzungumzia kinara huyo anayetafutwa na kikosi hicho, pamoja na kwamba Mratibu Mande hakumtaja kwa jina lake.
Uchunguzi  huo unaendeshwa chini ya kikosi hicho kinachojumuisha vyombo vya usalama kwa kushirikiana na vikosi vya kuzuia ujangili, katika Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro (NCAA),Hifadhi ya Manyara, Serengeti na Tarangire.
“Kundi la kwanza linahusisha wakazi wa kando kando mwa  hifadhi wanaofahamu mazingira, hivyo wanatoa taarifa mbalimbali kuhusu hifadhi na wanyamapori,” alisema  Mande. Alisema kundi la pili ni wataalam wa utumiaji silaha za moto maarufu kama ‘Sharp Shooter’ kwa kuwa wanakabidhiwa risasi kulingana na idadi ya wanyama wanaotakiwa kuuawa.
Alilitaja kundi la tatu, kuwa ni madalali wanaofanyakazi ya kuwasiliana na  kundi la nne, ambalo kimtandao linajengewa uwezo mkubwa kiuchumi kwa sababu ndilo linalowasiliana moja kwa moja na majangili wa kundi la tano, ambao ni vinara kwa hapa nchini.
“Majangili walioko  kwenye kundi la nne wamegawanywa katika kanda, wanawezeshwa kiuchumi baadhi wamenunuliwa magari aina ya Nissan Patrol ili kuwarahisishia utendaji hata inapotokea kukamatwa, nguvu kubwa hutumika kuvuruga kesi dhidi yao,” alieleza Mande. Mande alisema kundi la tano wanapokea oda na ufadhili kutoka kwa kundi la sita ambao wapo nchi za nje na kuwasilisha kwa mawakala wao ambao ni kundi la nne kwa ajili ya utekelezaji kupitia makundi yaliyotajwa.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments: