Chama cha Wafanyabiashara wa Viwanda na Kilimo
(TCCIA), mkoani Morogoro kimesema baadhi ya sheria ndogo zinazotungwa na
halmashauri, zimekuwa zikiwakandamiza wafanyabiashara na kusababisha
migogoro baina yao na vyombo vingine vya Serikali.
Hayo yalisemwa juzi na Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Morogoro, Bachoo Sidik wakati akifungua mdahalo wa wafanyabiashara na wadau wengine wa sekta ya kilimo cha biashara ulioandaliwa na East Africa Business Media Training Institute (EABMTI) na kufadhiliwa na Taasisi ya Biashara na Mazingira (Best Diologue).
Hayo yalisemwa juzi na Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Morogoro, Bachoo Sidik wakati akifungua mdahalo wa wafanyabiashara na wadau wengine wa sekta ya kilimo cha biashara ulioandaliwa na East Africa Business Media Training Institute (EABMTI) na kufadhiliwa na Taasisi ya Biashara na Mazingira (Best Diologue).
Bachoo alisema baadhi ya sheria hizo ni pamoja na
sheria na ulipiaji mabango ya biashara, ambapo wafanyabiashara hutakiwa
kuyalipia na wasipofanya hivyo huvunjwa au kuondolewa. Alisema sheria hiyo ndogo ya halmashauri
inapingana na sheria mama ya biashara iliyotungwa na Bunge, inayomtaka
mfanyabiashara kuweka bango linalotambulisha bidhaa au huduma anazotoa
bila malipo yoyote.
Bachoo alisema kutokana na mkanganyiko wa sheria
hizo, wafanyabiashara wamejikuta kwenye migogoro na halmashauri ambayo
huvunja mabango yasiyolipiwa. Akichangia, mfanyabiashara Shabani Kaigai alisema
ukadiriaji wa kodi TRA umekuwa kero kutokana na ukweli kuwa makadirio
hayaendani na kipato halisi cha wafanyabishara.
Alisema kuwa TRA wamekuwa wakikadiria kodi kubwa
na kusababsisha wafanyabiashara kufunga biashara zao, huku wengine
wakitoa rushwa ili kupunguziwa kodi ama kukwepa kuilipa kabisa. Ofisa Kodi wa TRA Mkoa wa Morogoro, Bashiru
Kahenaki alikiri kupanda kwa kodi. Hata hivyo, alisema TRA imekuwa
ikiwashauri wafanyabiashara kuwa na taarifa sahihi za biashara zao,
ikiwa ni pamoja vitabu vya risiti vinavyoonyesha mauzo yaliyofanyika.
Alisema wafanyabiashara wengi hawawasilishi
taarifa zao kupitia vitabu vya risiti, huku baadhi wakikosa uaminifu na
kukwepa kulipa kodi. Awali, Mkuu wa mdahalo huo kutoka EABMTI, Rosemary
Mwakitwange alisema mdahalo unaendeshwa ili kubaini changamaoto za
mazingira ya biashara na vipaumbele kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu wa
Oktoba.
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment