Pages

Tuesday, March 17, 2015

BANDARI YA TANGA YALALAMIKIA VITENDEA KAZI

Bandari ya Tanga inadaiwa kukabiliwa na changamoto ya utendaji hafifu wa Shirika la Reli na kuchangia kwa kiwango kikubwa kuhamishwa kwa shehena nyingi iliyokuwa ikipitia katika bandari hiyo, hasa iliyokuwa ikienda na kutoka Kanda ya Ziwa.

Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga, Moshi Mtambalike alisema kuwa, tangu 2009 hakuna shehena iliyosafirishwa kwa njia ya reli hadi sasa. Mtambalike alisema hayo wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi wa Bandari ya Tanga katika kipindi cha mwaka 2013/14 kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC). Alisema mtiririko wa meli na shehena kwa mwaka 2012/13 ulikuwa na jumla ya meli za kimataifa 83 na za mwambao 140, wakati kwa mwaka 2013/14 zilikuwa meli za kimataifa 68 na za mwambao 41.
Alitaja mabadiliko ya teknolojia ya muundo wa meli nyingi mpya ambazo zinajengwa bila kuwekwa vifaa vya kupakulia mizigo kuwa ni tatizo jingine.
Alisema kina kidogo cha maji kinachofanya meli kubwa kushindwa kutia nanga kinasababisha kuhudumia shehena mbili kwa wakati mmoja na kudai kuwa Mamlaka ya Bandari inatafakari namna ya kupata treni inayoelea ili kumaliza changamoto hizo.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula alimwomba meneja huyo kutolea ufafanuzi wa madai ya kuwapo kwa urasimu unaosababisha wateja kuacha kutumia bandari hiyo, suala alilokanusha. na kusema kwa sasa wamejipanga kutoa huduma bora kwa wateja wao licha kuwapo kwa changamoto hizo.

CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment