Pages

Thursday, January 22, 2015

TRA YAAGIZWA KUHARAKISHA UKAGUZI WA SUKARI NCHINI

Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imeiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuharakisha agizo la ukaguzi wa sekta ndogo ya sukari ili kupata ufumbuzi wa haraka.

Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe, akitoa maamuzi mara baada ya kuhojiana na TRA, alisema uingizwaji holela wa sukari una hatari kwa ukuaji wa viwanda vya ndani. “Tunataka taarifa ili tuweze kuwa na mikakati endelevu ya kuzuia sukari ya magendo, unasababaisha sukari inayozalishwa na viwanda vyetu na miwa ya wakulima ina kosa soko,” alibainisha.
Hivi karibuni, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janeth Mbene, alipotembelea kiwanda cha sukari cha TPC mkoani Kilimanjaro, alielezwa jinsi sukari ya nje iliyojaa sokoni na wao kukosa pa kuiuza. Alisema watakutana na Wizara zinazohusika kujadili na kuanza operesheni maalum kwenye maduka mbalimbali na kukamatwa sukari ya nje na ya viwandani inayouzwa kwa wananchi kwa bei ndogo.

CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment