Je, Chama cha Mapinduzi, CCM, kilipoamua
kuruhusu mfumo wa vyama vingi kilikuwa na wazo kwamba Chama kingine
kinaweza kukiangusha? Je sasa kinaweza kukubali kushindwa kwenye
chaguzi zinazoendelea nchini?
Haya ni miongoni mwa maswali yasiyo na majibu
sahihi. Kiini cha maswali haya ni jinsi ambavyo chama hicho tawala na
serikali yake vinavyoudhibiti upinzani katika harakati zake za kutaka
kukiondoa madarakani.
Ni takribani miaka 20 sasa tangu kuruhusiwa kwa
mfumo wa vyama vingi nchini. Lakini kwa kipindi chote hicho wapinzani
wamekuwa na uwanja hafifu wa ushindani dhidi ya CCM.
Serikali kupitia vyombo vya dola imekuwa ikiweka
mazingira magumu ya ushindi kwa kambi ya upinzani kuanzia ndani ya Tume
ya Uchaguzi ambayo imekuwa chini ya viongozi ambao sio tu wanateuliwa na
Mwenyekiti wa CCM, lakini wenyewe huwa makada wa chama hicho
kinachotawala.
Majibu ya maswali haya yanaainishwa na muasisi na
kiongozi mkongwe wa Chama hicho tawala mzee Isakwisa Mwambulukutu
Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Mbeya.
Mwambulukutu aliyejizolea umaarufu mkubwa enzi za
uongozi wake anaeleza msimamo wake kupitia mahojiano maalumu
yaliyofanywa na Mwandishi wa gazeti la Mwananchi wa mkoa wa Mbeya,
Lauden Mwambona.
Swali: Je CCM ilipoamua kuruhusu mfumo wa
vyama vingi , ilifikiria na kujiweka tayari kuondoka madarakani kama
itatokea kikashindwa kwenye uchaguzi?
Jibu: Ndiyo ilijua inaweza
kuondoka madarakani, lakini sasa nadhani haitakubali kuwaachia madaraka
wapinzani wenye matusi. Mimi naamini kama vyama vya upinzani
vitaendelea na mwelekeo wa sasa wa matusi na kutishia kumwaga damu, CCM
itakuwapo madarakani miaka mingine 50 ijayo.
Kinachoonekana sasa kwa viongozi wa vyama vya
upinzani ni kwamba wanatafuta kula, siyo uongozi wa nchi. Wanapenda
matusi na kutamka kauli za kumwaga damu jambo ambao sio tu CCM pekee
inayolipinga, bali hakuna mtanzania atakayekubali nchi itumbukie huko.
Lakini vyama vya upinzani vikijirekebisha na
kuingia kwenye uchaguzi kwa ustaarabu na kuacha kauli mbaya, CCM itakuwa
tayari kuondoka madarakani.
Swali: Awamu ya nne ya utawala wa CCM chini ya Rais Jakaya Kikwete itamalizika mwakani, je mambo gani wewe unaweza kusema unaona Rais Kikwete kayafanya vyema na ni wapi amekosea.
Jibu: Kwa kweli namshukuru Mungu
kwamba nimeshuhudia kazi zilizofanywa na viongozi wakuu nchini kuanzia
awamu ya kwanza hadi ya nne. Kila awamu zipo kazi kubwa zilizofanyika.
Swali: Tunaelekea kwenye uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwakani. Wapo wana CCM waliotangaza nia zao za kugombea Urais. Nini maoni yako kuhusu wanaCCM waliotangaza nia.
Swali: Kwa nini wazee waasisi wa siasa mkoani Mbeya hamjitokezi kuzungumza na vyombo vya habari kuhusu masuala ya nchi?
Swali: Kwani siku hiyo mlizungumzia kitu gani?
Hali kadhalika Rais Kikwete amefanya kazi nyingi za kuonekana .
Kwa mfano kajenga heshima kwa Tanzania kutambuliwa na mataifa
mbalimbali duniani.
Rais Kikwete ameweza kuwakaribisha marais wa
Mataifa makubwa duniani kama Barack Obama wa Marekani, Rais Xi Jiping
wa China wamefika hapa katika taifa ambalo ni maskini. Mpaka sasa marais
wastaafu wengi wa nchi hizo wanafika. Lakini pia Rais Kikwete amefanya makubwa katika
kujenga barabara za lami. Nchi sasa imeunganishwa kwa lami maeneo
mengi. Hali kadhalika Watanzania wengi wameshuhudia umeme ukisambaa
vijijini. Na hata maji yamesambazwa sana vijijini.
Rais Kikwete pia atakumbukwa sana kwa kujenga
shule za sekondari na vyuo vikuu vingi kuliko wengine wote. Wapo
wanaokosoa shule za kata, lakini fikiria zisingekuwapo shule hizo,
watoto hao wangekuwa wapi? Kikwete sasa anaendelea na mradi wa gesi ya Mtwara
na Lindi ambayo bila shaka itaongeza kasi ya maendeleo nchini . Lakini
siasa za uongo zilisema gesi inapelekwa Bagamoyo, jambo ambalo ni
propaganda za wapinga maendeleo. Kwa upande wa kasoro, mimi naamini kila binadamu
anao udhaifu ambacho Mungu alimpatia. Kwa mfano naona Rais Kikwete ni
mpole sana, hana ukali, lakini wengine wamegeuza upole wa rais wakisema
ni udhaifu, sawa, pengine huu ndio udhaifu wake.
Swali: Tunaelekea kwenye uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwakani. Wapo wana CCM waliotangaza nia zao za kugombea Urais. Nini maoni yako kuhusu wanaCCM waliotangaza nia.
Jibu: Kwa bahati nzuri mimi ni
mwanaCCM na nitakufa nikiwa CCM. Mimi naamini mgombea wa CCM bado. Hao
waliojitangaza hawanisumbui kabisaa. Sina mgombea, bali nasubiri
atakayeteuliwa na CCM tu.
Lakini kikubwa kwa CCM lazima ateuwe mgombea safi,
mwadilifu, mpenda watu, asiyeguswa na kashfa za aina yoyote ile .
Mteule wa CCM lazima awe yule anayependwa na Watanzania wote wakiwamo
wa Upinzani na ambaye anaogopwa na kambi ya upinzani.
Katika uongozi wa nchi hawatakiwi watu wapenda
rushwa wenye makundi bali sasa anatakiwa kiongozi mwenye hekima,
mwadilifu wa hali ya juu mzoefu katika siasa za ndani na za kimataifa.
Kwa kweli naamini mgombea wa CCM mwaka kesho atakuwa msafi anayependwa na Watanzania wote.
Swali: Kwa nini wazee waasisi wa siasa mkoani Mbeya hamjitokezi kuzungumza na vyombo vya habari kuhusu masuala ya nchi?
Jibu: Hapana hatujakaa kimya. Tuliwahi kuwaomba
waandishi kupitia umoja wenu, na tulikaa nao Mbeya Peak Hotel ambapo
tulizungumzia mchakato wa Katiba Mpya, lakini habari zetu hazikutoka .
Baadaye niliambiwa kwamba habari hazikutoka kwa
sababu waandishi wa siku hizi wanataka fedha kwanza. Nakumbuka ni
gazeti moja tu ndilo lililoandika ingawa waliofika walikuwa vijana wengi
wakiwamo wajukuu wangu.
Swali: Kwani siku hiyo mlizungumzia kitu gani?
Jibu: Kipindi hicho, Wazee wa
Mbeya tulikuwa na mambo mawili ambayo pamoja na kuwalaumu Wabunge
waliokuwa wakiwakashfu waasisi wa Taifa hili, hayati Baba wa Taifa
Mwalimu Julius Nyerere na Marehemu Abeid Aman Karume. Pia tulitaka
tumshauri Jaji msomi Joseph Warioba aache kulijibu Bunge lilipokuwa
likijadili rasimu ya Katiba Mpya.
Jaji Warioba na wajumbe wa Tume walifanya kazi
nzuri na kuikabidhi kwa Rais Jakaya Kikwete, hivyo sisi wazee tulitaka
tumshauri Jaji kwamba atulie wala asiingilie mjadala wa wabunge.
CHANZO: MWANANCHI
CHANZO: MWANANCHI
No comments:
Post a Comment