Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan 
Serikali
 nchini Nigeria inasema inachunguza taarifa ya idadi kubwa ya wanawake 
na wasichana waliotekwa nyara na wanamgambo wa Boko Haram Kaskazini 
Mashariki mwa nchi hiyo, pamoja na kwamba tangazo la kusitisha mapigano 
lililotolewa na majeshi ya serikali.
Msemaji wa Serikali ya 
Nigeria Mike Omeri, ameiambia BBC kuwa serikali ya Nigeria inajaribu 
kuthibitisha kile kilichotokea. Mwanakijiji mmoja anasema wanawake na 
wasichana arobaini wametekwa na kundi hilo.
Makubaliano ya kusitisha mapigano yalitangazwa wiki iliyopita, lakini mashambulizi yanaendelea na mpaka sasa haijajulikana kama wasichana wa Chibok zaidi ya mia mbili waliotekwa na kundi la Boko Haram miezi sita iliyopita wataachiwa huru kama serikali ya Nigeria ilivyosema.
CHANZO: BBC Swahili
    
Makubaliano ya kusitisha mapigano yalitangazwa wiki iliyopita, lakini mashambulizi yanaendelea na mpaka sasa haijajulikana kama wasichana wa Chibok zaidi ya mia mbili waliotekwa na kundi la Boko Haram miezi sita iliyopita wataachiwa huru kama serikali ya Nigeria ilivyosema.
CHANZO: BBC Swahili
No comments:
Post a Comment